Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
5Кб
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Поиск
Категории
Больше
2 KINGS
Verse by verse explanation of 2 Kings 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 40 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-03-19 19:23:59 0 5Кб
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 29
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 22 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-24 15:21:37 0 6Кб
MAHUSIANO KIBIBLIA
BIBLIA NA URAFIKI, UCHUMBA HADI NDOA
Bila shaka utaungana nami kuwa hakuna kipindi kinachosumbua katika maisha kama kipindi cha ujana,...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-06 11:31:28 0 6Кб
URAFIKI KIBIBLIA
JE, NITAJUAJE KAMA YUPO KWA AJILI YA NGONO AU KWA AJILI YA NDOA?
Hili ni miongoni mwa swali ninaloulizwa na mabinti wengi sana. Kwa hiyo nimeona ni muhimu sana...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-07 22:23:57 0 6Кб
HOLY BIBLE
Responding to the Jehovah’s Witness attacks on the deity of Christ
If Jesus is God, why did he pray to the Father in John 17? Jesus prayed to the Father because as...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:00:07 0 6Кб