Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
5K
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Cerca
Categorie
Leggi tutto
Injili Ya Yesu Kristo
DINI YA KIISLAM ILIANZISHWA SIKU YA JUMATATU MWEZI WA 17, SAWA SAWA NA TAREHE 27 DESEMBA MKWA 610 B.K.
KUMBE UISLAM NI DINI YA KUTENGEZA TU, TENA CHANGA SANA NA HAIKUWEPO KABLA YA MUHAMMAD  ...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:13:31 0 5K
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 34
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 15:36:59 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
Yesu alikuwa wapi katika siku tatu toka siku ile ya kufa mpaka kufufuka?
Kama Yesu alivyotabiri, alisalitiwa na mmoja wa wafuasi wake, Yuda Iscariot, na alikamatwa....
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:39:59 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
IPONYE NAFSI YAKO, EPUKA MANABII WA UONGO
Muhubiri/ Mtumishi yeyote aliyerudi nyuma na kusahau kusudi lake tayari anageuka kuwa nabii wa...
By GOSPEL PREACHER 2023-06-17 23:43:15 0 8K
HOLY BIBLE
Did Jesus fight Satan for the keys to the kingdom?
Keys are a symbol of control. Keys keep people in or out. If they do not have a key to a lock,...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:21:41 0 6K