Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
6K
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
REVELATION
UFUNUO 18
Tukirejea kwenye ile sura ya 17 tunamwona yule mwanamke KAHABA aliyeketi juu ya yule...
By GOSPEL PREACHER 2021-10-30 12:17:39 0 6K
NDOA KIBIBLIA
NDOA YA MKE MMOJA NA MUME MMOJA NI AGIZO NA NI SHERIA YA MUNGU
UTANGULIZI:Kumekuwepo na mkanganyiko mkubwa katika swala la ndoa kati ya ndoa ya mke...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:04:02 0 8K
MAHUSIANO KIBIBLIA
KWA NINI WATU WENGI WANAUMIA BAADA YA KUINGIA KWENYE MAHUSIANO?
Kumekuwa na takwimu nyingi za wachumba na wanandoa kuumia mara tu au muda mfupi baadaye baada ya...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 14:52:10 0 5K
UCHUMBA KIBIBLIA
KANUNI 10 ZA UCHUMBA WENYE KUFANIKIWA
KwanzaWewe na mwenzako mnaweza kuwa na sifa nyingi kama wachumba. Huenda mkijitazama na watu...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 10:32:02 0 6K
SPIRITUAL EDUCATION
Why Do Bad Things Happen To Good People?
If God is completely in control, why do our lives sometimes not turn out as planned? If God is...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:22:09 0 5K