Bwana Aliposema Kuwa Yeye Ni “Mungu Wa Miungu” Alikuwa Na Maana Gani?..Je! Yeye Ni Mungu Wa Sanamu?

0
6K

JIBU: Tukisoma Kumbukumbu 10:17 inasema…

“Kwa maana Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu wa miungu, na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye kuogofya, asiyependelea nyuso za watu, wala hakubali rushwa”.  

Hapa tunaona Mungu anajitambulisha yeye kama “Mungu wa miungu” sasa swali hawa miungu ni wakina nani?.   Bwana Yesu alisema mahali fulani katika kitabu cha Yohana,..  

Yohana 10:33 “Wayahudi wakamjibu, Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu. 34 Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka); 36 je! Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?”  

Kwahiyo unaona hapo miungu inayozungumziwa hapo ni WATOTO WA MUNGU, (yaani sisi tuliomwamini yeye na kuoshwa kwa damu yake) inadhaniwa na wengi kuwa miungu iliyozungumziwa pale ni “SANAMU” LA! sivyo. Mungu hawezi akawa ni Mungu wa sanamu. Sanamu hata siku moja haziwezi zikampa Mungu utukufu, Na tunajua tabia za miungu ni lazima zifanane na Mungu, Hivyo basi kazi zile zile Mungu anazozifanya lazima na miungu izifanye, kwa mfano Mungu alitumia NENO lake kuumba na kufanya kila kitu na sisi vivyo hivyo kwa NENO lake tunaweza tukafanya kazi za Mungu vile vile kama yeye. Lakini tusipoweza kufanya hivyo inamaana sisi sio miungu kwasababu hatufanani na yeye. ni sawasawa tu na alivyojiita yeye ni MFALME wa wafalme, au BWANA wa mabwana.  

Kwahiyo ili sisi tuwe miungu lazima tuwe ni WATOTO WA MUNGU wenye tabia kama za kwake nazo ni: Upendo, Imani, Haki, Utakatifu, utu wema, kiasi n.k Wagalatia 5:22 hivyo tuzidi kutia bidii katika kumjua yeye ili tustahili kuitwa miungu.  

Maelezo haya unaweza kuyapata kwa njia ya video mwisho wa somo hili

Ubarikiwe sana.  

Căutare
Categorii
Citeste mai mult
Networking
KARIBU PROSHABO.COM TUHUBIRI INJILI PAMOJA
KWA MASWALI AU MAONI, BONYEZA HAPA? Bwana Yesu asifiwe!! Karibu sana PROSHABO.COM, kwa pamoja...
By PROSHABO NETWORK 2021-09-04 09:51:34 3 6K
Networking
How to choose the right marketplace business model
To build a sustainable and successful marketplace platform, you need to find a business model...
By Business Academy 2022-09-17 03:32:43 0 6K
OTHERS
What was God doing before He created the universe?
Our finite minds find it hard to comprehend that before the universe was created, God existed...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:38:19 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Ushuhuda wa Victoria Juu ya Kuzimu
Huu ni ufupisho wa ushuhuda wa Victoria Nehale Nilizaliwa na kuishi Namibia maisha yangu yote;...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:40:22 0 5K
CHRISTIAN EDUCATION
WEWE NI HEKALU LA MUNGU
WEWE NI HEKALU LA MUNGU 
By Martin Laizer 2023-12-23 16:13:51 0 7K