Bwana Aliposema Kuwa Yeye Ni “Mungu Wa Miungu” Alikuwa Na Maana Gani?..Je! Yeye Ni Mungu Wa Sanamu?

0
6KB

JIBU: Tukisoma Kumbukumbu 10:17 inasema…

“Kwa maana Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu wa miungu, na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye kuogofya, asiyependelea nyuso za watu, wala hakubali rushwa”.  

Hapa tunaona Mungu anajitambulisha yeye kama “Mungu wa miungu” sasa swali hawa miungu ni wakina nani?.   Bwana Yesu alisema mahali fulani katika kitabu cha Yohana,..  

Yohana 10:33 “Wayahudi wakamjibu, Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu. 34 Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka); 36 je! Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?”  

Kwahiyo unaona hapo miungu inayozungumziwa hapo ni WATOTO WA MUNGU, (yaani sisi tuliomwamini yeye na kuoshwa kwa damu yake) inadhaniwa na wengi kuwa miungu iliyozungumziwa pale ni “SANAMU” LA! sivyo. Mungu hawezi akawa ni Mungu wa sanamu. Sanamu hata siku moja haziwezi zikampa Mungu utukufu, Na tunajua tabia za miungu ni lazima zifanane na Mungu, Hivyo basi kazi zile zile Mungu anazozifanya lazima na miungu izifanye, kwa mfano Mungu alitumia NENO lake kuumba na kufanya kila kitu na sisi vivyo hivyo kwa NENO lake tunaweza tukafanya kazi za Mungu vile vile kama yeye. Lakini tusipoweza kufanya hivyo inamaana sisi sio miungu kwasababu hatufanani na yeye. ni sawasawa tu na alivyojiita yeye ni MFALME wa wafalme, au BWANA wa mabwana.  

Kwahiyo ili sisi tuwe miungu lazima tuwe ni WATOTO WA MUNGU wenye tabia kama za kwake nazo ni: Upendo, Imani, Haki, Utakatifu, utu wema, kiasi n.k Wagalatia 5:22 hivyo tuzidi kutia bidii katika kumjua yeye ili tustahili kuitwa miungu.  

Maelezo haya unaweza kuyapata kwa njia ya video mwisho wa somo hili

Ubarikiwe sana.  

Rechercher
Catégories
Lire la suite
DANIEL
DANELI 3
Jina la Bwana wetu na Mkuu wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu katika mwendelezo wa kitabu...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-05 23:37:05 0 7KB
OTHERS
JEHANNAM NI NYUMBA YA MILELE YA WAISLAM
JEHANAMU IPO NA INASUBIRI WATENDA DHAMBI Huko motoni Jehanum kukoje? Mwanangu, kunatisha,...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:29:42 0 5KB
NDOA KIBIBLIA
NDOA YA MKE MMOJA NA MUME MMOJA NI AGIZO NA NI SHERIA YA MUNGU
UTANGULIZI:Kumekuwepo na mkanganyiko mkubwa katika swala la ndoa kati ya ndoa ya mke...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:04:02 0 7KB
MASWALI & MAJIBU
KUZIMU Ni Mahali Pa Namna Gani, Je! Huko Wanaishi Watu Wakifa Na Kwenda Kupata Mateso Au Ni Vinginevyo?
JIBU: Kuzimu ipo, na ni sehemu iliyo halisi kabisa biblia inaelezea katika (Luka...
Par GOSPEL PREACHER 2022-06-13 09:15:09 0 6KB
REVELATION
MAJIRA YA KANISA LA SMIRNA
Majira haya ya kanisa la Smirna tutayaona katika {UFUNUO 2:8 -11} ambapo kama...
Par GOSPEL PREACHER 2021-09-24 08:49:32 0 6KB