Bwana Aliposema Kuwa Yeye Ni “Mungu Wa Miungu” Alikuwa Na Maana Gani?..Je! Yeye Ni Mungu Wa Sanamu?

0
6K

JIBU: Tukisoma Kumbukumbu 10:17 inasema…

“Kwa maana Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu wa miungu, na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye kuogofya, asiyependelea nyuso za watu, wala hakubali rushwa”.  

Hapa tunaona Mungu anajitambulisha yeye kama “Mungu wa miungu” sasa swali hawa miungu ni wakina nani?.   Bwana Yesu alisema mahali fulani katika kitabu cha Yohana,..  

Yohana 10:33 “Wayahudi wakamjibu, Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu. 34 Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka); 36 je! Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?”  

Kwahiyo unaona hapo miungu inayozungumziwa hapo ni WATOTO WA MUNGU, (yaani sisi tuliomwamini yeye na kuoshwa kwa damu yake) inadhaniwa na wengi kuwa miungu iliyozungumziwa pale ni “SANAMU” LA! sivyo. Mungu hawezi akawa ni Mungu wa sanamu. Sanamu hata siku moja haziwezi zikampa Mungu utukufu, Na tunajua tabia za miungu ni lazima zifanane na Mungu, Hivyo basi kazi zile zile Mungu anazozifanya lazima na miungu izifanye, kwa mfano Mungu alitumia NENO lake kuumba na kufanya kila kitu na sisi vivyo hivyo kwa NENO lake tunaweza tukafanya kazi za Mungu vile vile kama yeye. Lakini tusipoweza kufanya hivyo inamaana sisi sio miungu kwasababu hatufanani na yeye. ni sawasawa tu na alivyojiita yeye ni MFALME wa wafalme, au BWANA wa mabwana.  

Kwahiyo ili sisi tuwe miungu lazima tuwe ni WATOTO WA MUNGU wenye tabia kama za kwake nazo ni: Upendo, Imani, Haki, Utakatifu, utu wema, kiasi n.k Wagalatia 5:22 hivyo tuzidi kutia bidii katika kumjua yeye ili tustahili kuitwa miungu.  

Maelezo haya unaweza kuyapata kwa njia ya video mwisho wa somo hili

Ubarikiwe sana.  

Căutare
Categorii
Citeste mai mult
OTHERS
Allah is never found in the Bible
  I. Allah is never found in the BibleContrary to Muslim claims, the word "Allah" is never...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:50:33 0 9K
Injili Ya Yesu Kristo
MSHINDE GOLIATHI.
Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi; Goliathi alikuwa ni mtu wa vita wa kifilisti. Habari za mtu...
By GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:03:54 0 5K
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 24
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 58 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:34:42 0 5K
GENESIS
GENESIS 1 : VERSE BY VERSE EXPLANATION
Verses 1:1 – 2:3: This description of God creating heaven and earth is understood to be:...
By MOCARECI CHURCH 2021-12-05 22:43:49 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
NAMNA YA KUMWITA,KWENDA NA KUMUOMBA MUNGU ILI AKUSIKILIZE.
Yeremia 29:12 “Nanyi mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami nitawasikiliza”....
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:21:47 0 5K