KWANINI SULEIMAN ALIKUWA NA WAKE MIA SABA (700) NA MASURIA MIA TATU (300)?

0
6K
Kwenye 1 WaFalme 11:1-3, kwa nini Suleiman alikuwa na wake 700 na Masuria 300, kinyume cha amri ya Mungu ya kwenye Kumb 17:17?
 
Jibu: Kumbukumbu 17:17 inasema mfalme asiwe na wake wengi, na kwa kitendo hicho, Suleiman alifanya dhambi. Kuoa wake ilikuwa ni njia ya kuimarisha ushirikiano na falme nyingine, lakini pia ilikuwa ni makosa kutokumtii Mungu. 1 Fal 11:1-4 inasema kuwa Suleiman alifanya dhambi kwa kuoa hawa wake wageni, na kuugeuzia moyo wake kuwa mbali na Mungu.
 
Hard Sayings of the Bible uk.229 inalitumia jambo hili kwa njia ya kupendeza sana. Ingawa Suleiman angeweza kuweka viwango vya juu kama mfano, alianza kujiona kama hana haja ya kuzuiliwa na Mungu kwa njia hii. Leo hii kama kiongozi wa kikristo anajiona kuwa hayumo kwenye mipaka ambayo Mungu ameiweka kwa Wakristo wa kawaida, kiongozi huyu atakuwa kwenye shida kubwa sana ya kiroho. Kwenye Kurani, hakuna mwanaume anayeruhusiwa kuwa na zaidi ya wake wanne, isipokuwa Muhammad tu, ambaye alitokea kuwa na wake karibu 24 baada ya Khadija, na Masuria kumi na wawili.
 
Zaidi ya hayo, Muhammad na Waislam wengine walikuwa na wasichana mateka na watumwa, na Kurani inawaruhusu Waislam kufanya tendo la ndoa na wanawake ambao wanawamiliki kwa nguvu ya mikono yao. (Sura 4:24; 23:5-6; 70:29-30; 33:50,52 Abu Dawud juzuu ya 2 na.2150 uk.577)
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom
Like
1
Căutare
Categorii
Citeste mai mult
2 SAMUEL
Book of 2 Samuel Explained
Introduction: See 1 Samuel for the introductory discussion. First and Second Samuel were...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-27 20:29:09 0 6K
EZRA
Verse by verse explanation of Ezra 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-02 06:07:58 0 6K
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 62 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 09:44:08 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
YESU NI MWANA WA MUNGU
Je, ina maana gani Yesu kuwa Mwana wa Mungu    Ndugu Msomaji, Yesu si Mwana wa Mungu...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:24:13 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
MASWALI YA KITABU CHA MWANZO
MASWALI YA KITABU CHA MWANZO KWA WATOTO Nani alimwuzia mwenzake haki ya...
By PROSPER HABONA 2024-01-07 04:56:40 0 4K