KWANINI SULEIMAN ALIKUWA NA WAKE MIA SABA (700) NA MASURIA MIA TATU (300)?

0
5χλμ.
Kwenye 1 WaFalme 11:1-3, kwa nini Suleiman alikuwa na wake 700 na Masuria 300, kinyume cha amri ya Mungu ya kwenye Kumb 17:17?
 
Jibu: Kumbukumbu 17:17 inasema mfalme asiwe na wake wengi, na kwa kitendo hicho, Suleiman alifanya dhambi. Kuoa wake ilikuwa ni njia ya kuimarisha ushirikiano na falme nyingine, lakini pia ilikuwa ni makosa kutokumtii Mungu. 1 Fal 11:1-4 inasema kuwa Suleiman alifanya dhambi kwa kuoa hawa wake wageni, na kuugeuzia moyo wake kuwa mbali na Mungu.
 
Hard Sayings of the Bible uk.229 inalitumia jambo hili kwa njia ya kupendeza sana. Ingawa Suleiman angeweza kuweka viwango vya juu kama mfano, alianza kujiona kama hana haja ya kuzuiliwa na Mungu kwa njia hii. Leo hii kama kiongozi wa kikristo anajiona kuwa hayumo kwenye mipaka ambayo Mungu ameiweka kwa Wakristo wa kawaida, kiongozi huyu atakuwa kwenye shida kubwa sana ya kiroho. Kwenye Kurani, hakuna mwanaume anayeruhusiwa kuwa na zaidi ya wake wanne, isipokuwa Muhammad tu, ambaye alitokea kuwa na wake karibu 24 baada ya Khadija, na Masuria kumi na wawili.
 
Zaidi ya hayo, Muhammad na Waislam wengine walikuwa na wasichana mateka na watumwa, na Kurani inawaruhusu Waislam kufanya tendo la ndoa na wanawake ambao wanawamiliki kwa nguvu ya mikono yao. (Sura 4:24; 23:5-6; 70:29-30; 33:50,52 Abu Dawud juzuu ya 2 na.2150 uk.577)
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom
Like
1
Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
JOB
Verse by verse explanation of Job 5
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-02 13:33:02 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
NITAMTAMBUAJE MKE AMBAYE MUNGU AMENIANDALIA?
SwaliBwana Yesu asifiwe mtumishi wa Mungu.Awali ya yote napenda kumshukuru Mungu kwa ajili yenu...
από GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:20:18 0 4χλμ.
JOB
Verse by verse explanation of Job 17
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 20 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:32:17 0 5χλμ.
SPIRITUAL EDUCATION
The Holy Spirit's Comfort, Guidance and Help
In John, chapter 14, verses 15 to 17, Jesus said: "If ye love me, keep my commandments. And I...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 18:37:56 0 4χλμ.
OTHERS
LEO TUTAMTAZAMA BWANA YESU NA MUHAMAD NI NANI MWENYE MATUMAINI YENYE UHAKIKA KATI YAO
Tutapitia kauli zao walizozisema wakiwa Duniani, na kila mmoja atahukumu ni yupi mbora wa kufwata...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 20:09:59 0 5χλμ.