KWANINI SULEIMAN ALIKUWA NA WAKE MIA SABA (700) NA MASURIA MIA TATU (300)?

0
5كيلو بايت
Kwenye 1 WaFalme 11:1-3, kwa nini Suleiman alikuwa na wake 700 na Masuria 300, kinyume cha amri ya Mungu ya kwenye Kumb 17:17?
 
Jibu: Kumbukumbu 17:17 inasema mfalme asiwe na wake wengi, na kwa kitendo hicho, Suleiman alifanya dhambi. Kuoa wake ilikuwa ni njia ya kuimarisha ushirikiano na falme nyingine, lakini pia ilikuwa ni makosa kutokumtii Mungu. 1 Fal 11:1-4 inasema kuwa Suleiman alifanya dhambi kwa kuoa hawa wake wageni, na kuugeuzia moyo wake kuwa mbali na Mungu.
 
Hard Sayings of the Bible uk.229 inalitumia jambo hili kwa njia ya kupendeza sana. Ingawa Suleiman angeweza kuweka viwango vya juu kama mfano, alianza kujiona kama hana haja ya kuzuiliwa na Mungu kwa njia hii. Leo hii kama kiongozi wa kikristo anajiona kuwa hayumo kwenye mipaka ambayo Mungu ameiweka kwa Wakristo wa kawaida, kiongozi huyu atakuwa kwenye shida kubwa sana ya kiroho. Kwenye Kurani, hakuna mwanaume anayeruhusiwa kuwa na zaidi ya wake wanne, isipokuwa Muhammad tu, ambaye alitokea kuwa na wake karibu 24 baada ya Khadija, na Masuria kumi na wawili.
 
Zaidi ya hayo, Muhammad na Waislam wengine walikuwa na wasichana mateka na watumwa, na Kurani inawaruhusu Waislam kufanya tendo la ndoa na wanawake ambao wanawamiliki kwa nguvu ya mikono yao. (Sura 4:24; 23:5-6; 70:29-30; 33:50,52 Abu Dawud juzuu ya 2 na.2150 uk.577)
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom
Like
1
البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
Injili Ya Yesu Kristo
Ushuhuda wa Victoria Juu ya Kuzimu
Huu ni ufupisho wa ushuhuda wa Victoria Nehale Nilizaliwa na kuishi Namibia maisha yangu yote;...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:40:22 0 5كيلو بايت
REVELATION
MAJIRA YA KANISA LA THIATIRA
(1) MLENGWA WA KANISA{UFUNUO 2:18}Na kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika; Haya ndiyo...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-09-24 09:47:12 2 7كيلو بايت
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 25
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 40 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-26 04:18:25 0 6كيلو بايت
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
GFG
FDF
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-12-31 12:37:18 0 5كيلو بايت
MASWALI & MAJIBU
Kubatizwa kwa ajili ya wafu ndio kupi, kuonakozungumziwa katika 1 Wakoritho 15:29?
Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani? Swali linaendelea… kulingana na huu...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-06-12 23:32:15 0 5كيلو بايت