KWANINI SULEIMAN ALIKUWA NA WAKE MIA SABA (700) NA MASURIA MIA TATU (300)?
Posted 2021-12-24 21:03:13
0
5K
Kwenye 1 WaFalme 11:1-3, kwa nini Suleiman alikuwa na wake 700 na Masuria 300, kinyume cha amri ya Mungu ya kwenye Kumb 17:17?
Jibu: Kumbukumbu 17:17 inasema mfalme asiwe na wake wengi, na kwa kitendo hicho, Suleiman alifanya dhambi. Kuoa wake ilikuwa ni njia ya kuimarisha ushirikiano na falme nyingine, lakini pia ilikuwa ni makosa kutokumtii Mungu. 1 Fal 11:1-4 inasema kuwa Suleiman alifanya dhambi kwa kuoa hawa wake wageni, na kuugeuzia moyo wake kuwa mbali na Mungu.
Hard Sayings of the Bible uk.229 inalitumia jambo hili kwa njia ya kupendeza sana. Ingawa Suleiman angeweza kuweka viwango vya juu kama mfano, alianza kujiona kama hana haja ya kuzuiliwa na Mungu kwa njia hii. Leo hii kama kiongozi wa kikristo anajiona kuwa hayumo kwenye mipaka ambayo Mungu ameiweka kwa Wakristo wa kawaida, kiongozi huyu atakuwa kwenye shida kubwa sana ya kiroho. Kwenye Kurani, hakuna mwanaume anayeruhusiwa kuwa na zaidi ya wake wanne, isipokuwa Muhammad tu, ambaye alitokea kuwa na wake karibu 24 baada ya Khadija, na Masuria kumi na wawili.
Zaidi ya hayo, Muhammad na Waislam wengine walikuwa na wasichana mateka na watumwa, na Kurani inawaruhusu Waislam kufanya tendo la ndoa na wanawake ambao wanawamiliki kwa nguvu ya mikono yao. (Sura 4:24; 23:5-6; 70:29-30; 33:50,52 Abu Dawud juzuu ya 2 na.2150 uk.577)
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom

Zoeken
Categorieën
- BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
- SPIRITUAL EDUCATION
- MASWALI & MAJIBU
- WORLD'S EDUCATION
- MAHUSIANO KIBIBLIA
- Injili Ya Yesu Kristo
- OTHERS
Read More
Book of Numbers Explained
Introduction: Something went terribly wrong on the way to the Promised land. Why would it...
Alipita katikati yao Akaenda zake!
Luka 4:16-30 “Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; na siku ya sabato akaingia katika...
Ni nani atakayewashitaki wateule
Warumi 8:31-33 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu...
Who is Jesus Christ and what is His mission to the world?
Is certainly a logical question to ask. He changed the world in only 30 years on earth, and no...
SINAGOGI SIO MSIKITI
TUNAZIDI KUCHAMBUA HOJA ZA MIHADHARA ya Kiislamu
LEO TUANGALIE SINAGOGI!! Sehemu ya...