Kujichua/punyeto – je, ni dhambi kulingana na Biblia?

0
5كيلو بايت
Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.
 
Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.
 
Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.
البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 16
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 58 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:15:50 0 6كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
Ukijibu Kabla Haujasikia, Ni Upumbavu Na Aibu Kwako.
Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,  Ni upumbavu na aibu kwake. Hekima...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2023-09-22 19:28:42 0 6كيلو بايت
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-05-20 12:20:31 0 8كيلو بايت
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
5 Money Mistakes That Lead to Debt
Here are five common money mistakes that can quickly lead to debt. Avoid them at all costs. 1....
بواسطة BIBLICAL FINANCES 2021-12-29 15:51:36 0 10كيلو بايت
SPIRITUAL EDUCATION
KWANINI WENGINE WANYAKULIWE NA WENGINE WAACHWE
KWANINI WENGINE WANYAKULIWE NA WENGINE WAACHWE.
بواسطة Martin Laizer 2023-10-10 18:45:10 4 8كيلو بايت