Kujichua/punyeto – je, ni dhambi kulingana na Biblia?

0
5KB
Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.
 
Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.
 
Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
Injili Ya Yesu Kristo
MWANANGU, YULE MAMA HAKUMALIZA VIZURI SAFARI YAKE
Mwanangu yule mama hakumaliza vizuri safari yake! Hivi ndivyo Mchungaji wangu, alivyoanza...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:39:49 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
KUBOMOA MADHABAHU ZA SHETANI
Madhabahu ni nini? Ni daraja la kuunganisha katika ya ulimwengu wa roho wa Mungu au shetani. Kuna...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-19 07:26:43 0 7KB
SPIRITUAL EDUCATION
NI NINI KITAKACHOTUTENGA NA UPENDO YESU KRISTO?
NI NINI KITAKACHOTUTENGA NA UPENDO YESU KRISTO?WARUMI 8:35-39
Par Martin Laizer 2023-09-30 15:42:48 1 15KB
MASWALI & MAJIBU
Kati Ya Unyakuo, Dhiki Kuu, Utawala Wa Miaka 1000 Kipi Kinaanza?
SWALI:Naomba kuuliza kati ya Unyakuo wa watakatifu, Dhiki kuu, Vita vya har-magedoni, Utawala wa...
Par GOSPEL PREACHER 2022-06-13 09:09:30 0 6KB
DANIEL
DANIELI 2
Kulikuwa na sababu kwanini Mungu aliinyanyua Babeli kuwa taifa lenye nguvu kuliko yote duniani...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-05 23:30:33 0 10KB