Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
6Кб
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Поиск
Категории
Больше
HOLY BIBLE
THE HOLY BIBLE
Welcome to Proshabo Online Bible Study (POBS). This is the best platform for you to...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-01 08:57:05 0 8Кб
Networking
How to communicate your marketplace value proposition
People's attention spans have become shorter. With the rapid growth in the number of online...
От Business Academy 2022-09-17 03:45:17 0 10Кб
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 16
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 32 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:47:48 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
HAKIKISHA UNAISHI MAISHA ULIYOKUSUDIWA UKIJUA KUSUDI LA UWEPO WAKO LIMEFUNGWA KWENYE MUDA
Mtu hakuumbwa (hakuzaliwa) kwa bahati mbaya bali kwa kusudi maalum la Mungu. Mungu...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-23 13:05:23 0 6Кб
OTHERS
JE, MUHAMMAD ALIROGWA?
Leo napenda Kumnukuu Mwalimu wangu Daniel Mwankemwa katika majawapo ya Makala ambayo anaelezea...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:53:13 0 6Кб