Je! kuna dhambi kubwa na ndogo?

0
5K

SWALI: Naomba kufahamu Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?


JIBU: Dhambi ni dhambi iwe kubwa au ndogo, zote ni kosa, biblia inasema.

Yakobo 2:10 “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. 11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. “

Unaona hapo? Kwahiyo mtu akitenda dhambi iwe kubwa au ndogo ataadhibiwa. lakini adhabu zitatofautiana huko waendako kulingana na wingi wa makosa, kwasababu Bwana Yesu pia alisema aliyeua kwa upanga atauawa kwa upanga, apandacho mtu ndicho atakachovuna. adhabu ya shetani haiwezi ikawa sawa na adhabu ya mwanadamu. Biblia inaeleza..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, ATAPIGWA SANA. 48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, ATAPIGWA KIDOGO. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi. “

Kwahiyo mapigo yanatofautiana kulingana na matendo ya mtu aliyoyatenda akiwa hapa duniani, ni kama tu vile thawabu zitavyotofautiana kwa mtu na mtu mbinguni kwa jinsi alivyotaabika katika kumtumikia Bwana vivyo hivyo na jehanamu adhabu zitatofautiana kulingana na dhambi mtu alizotenda akiwa ulimwenguni. Na jinsi gani alivyoipuuzia neema ya wokovu.

Hivyo hatupaswi kuipima dhambi kwa namna yoyote, ni kukaa nayo mbali kwasababu iwe ni kubwa au ndogo mshahara wake ni MAUTI, Warumi 6:23.

Dhambi kubwa na ndoto zote zina adhabu ya mauti.

Je! Umempa Yesu maisha yako ndugu yangu? Unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho?. Ukifa leo utakuwa mgeni wa nani, huko uendako?. Tubu sasa mgeukie yeye atakusamehe, na kukupa uzima wa milele.

Mungu akubariki.

Pesquisar
Categorias
Leia Mais
Injili Ya Yesu Kristo
VUNJA VIFUNGO, MAAGANO, NA MIKATABA YA KISHETANI MAISHANI MWAKO
Kutoka 23:32 ''Usifanye maagano pamoja nao, wala pamoja na miungu yao.'' Agano ni kitu...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:28:44 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Mpango Wa Wokovu ni nini?
Una njaa? Si njaa ya chakula, lakini je, una njaa ya kitu Fulani zaidi maishani? Je, kuna hali...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:10:21 0 5K
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 62 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-24 09:44:08 0 5K
Networking
How to design your marketplace transaction flow
The marketplace transaction flow is complicated, but careful design can make it smooth and...
Por Business Academy 2022-09-17 03:40:25 0 9K
PSALMS
Book of Psalms Explained
Book of Psalms “Title”: The English title comes for the Septuagint, which...
Por THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:29:36 0 6K