Je! kuna dhambi kubwa na ndogo?

0
5KB

SWALI: Naomba kufahamu Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?


JIBU: Dhambi ni dhambi iwe kubwa au ndogo, zote ni kosa, biblia inasema.

Yakobo 2:10 “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. 11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. “

Unaona hapo? Kwahiyo mtu akitenda dhambi iwe kubwa au ndogo ataadhibiwa. lakini adhabu zitatofautiana huko waendako kulingana na wingi wa makosa, kwasababu Bwana Yesu pia alisema aliyeua kwa upanga atauawa kwa upanga, apandacho mtu ndicho atakachovuna. adhabu ya shetani haiwezi ikawa sawa na adhabu ya mwanadamu. Biblia inaeleza..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, ATAPIGWA SANA. 48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, ATAPIGWA KIDOGO. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi. “

Kwahiyo mapigo yanatofautiana kulingana na matendo ya mtu aliyoyatenda akiwa hapa duniani, ni kama tu vile thawabu zitavyotofautiana kwa mtu na mtu mbinguni kwa jinsi alivyotaabika katika kumtumikia Bwana vivyo hivyo na jehanamu adhabu zitatofautiana kulingana na dhambi mtu alizotenda akiwa ulimwenguni. Na jinsi gani alivyoipuuzia neema ya wokovu.

Hivyo hatupaswi kuipima dhambi kwa namna yoyote, ni kukaa nayo mbali kwasababu iwe ni kubwa au ndogo mshahara wake ni MAUTI, Warumi 6:23.

Dhambi kubwa na ndoto zote zina adhabu ya mauti.

Je! Umempa Yesu maisha yako ndugu yangu? Unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho?. Ukifa leo utakuwa mgeni wa nani, huko uendako?. Tubu sasa mgeukie yeye atakusamehe, na kukupa uzima wa milele.

Mungu akubariki.

Suche
Kategorien
Mehr lesen
JONAH
YONA 1
Yona alikuwa mmoja wa manabii wa Israeli wakati wa utawala wa Yeroboamu Mfalme wa Israeli,...
Von GOSPEL PREACHER 2022-01-20 03:02:57 0 8KB
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 37 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-02-05 12:32:39 0 5KB
MAHUSIANO KIBIBLIA
SEHEMU YA 3: MISINGI YA KIIMANI KATIKA MAHUSIANO YA UCHUMBA HADI NDOA
Bwana asifiwe!! Unaweza kusoma SEHEMU YA 1, SEHEMU YA 2, SEHEMU YA 4 au SEHEMU YA 5 ya somo hili,...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-06 11:43:23 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
UMEJIAANDAJE KWA TUKIO LA UNYAKUO? (Sehemu ya 1)
Nakusalimu kwa jina la Yesu! Ili uweze kuelewa somo hili mpenzi msomaji nakushauri tafuta muda...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-23 13:07:03 0 5KB
HOLY BIBLE
Did Jesus fight Satan for the keys to the kingdom?
Keys are a symbol of control. Keys keep people in or out. If they do not have a key to a lock,...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:21:41 0 5KB