Je! kuna dhambi kubwa na ndogo?

0
5Кб

SWALI: Naomba kufahamu Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?


JIBU: Dhambi ni dhambi iwe kubwa au ndogo, zote ni kosa, biblia inasema.

Yakobo 2:10 “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. 11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. “

Unaona hapo? Kwahiyo mtu akitenda dhambi iwe kubwa au ndogo ataadhibiwa. lakini adhabu zitatofautiana huko waendako kulingana na wingi wa makosa, kwasababu Bwana Yesu pia alisema aliyeua kwa upanga atauawa kwa upanga, apandacho mtu ndicho atakachovuna. adhabu ya shetani haiwezi ikawa sawa na adhabu ya mwanadamu. Biblia inaeleza..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, ATAPIGWA SANA. 48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, ATAPIGWA KIDOGO. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi. “

Kwahiyo mapigo yanatofautiana kulingana na matendo ya mtu aliyoyatenda akiwa hapa duniani, ni kama tu vile thawabu zitavyotofautiana kwa mtu na mtu mbinguni kwa jinsi alivyotaabika katika kumtumikia Bwana vivyo hivyo na jehanamu adhabu zitatofautiana kulingana na dhambi mtu alizotenda akiwa ulimwenguni. Na jinsi gani alivyoipuuzia neema ya wokovu.

Hivyo hatupaswi kuipima dhambi kwa namna yoyote, ni kukaa nayo mbali kwasababu iwe ni kubwa au ndogo mshahara wake ni MAUTI, Warumi 6:23.

Dhambi kubwa na ndoto zote zina adhabu ya mauti.

Je! Umempa Yesu maisha yako ndugu yangu? Unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho?. Ukifa leo utakuwa mgeni wa nani, huko uendako?. Tubu sasa mgeukie yeye atakusamehe, na kukupa uzima wa milele.

Mungu akubariki.

Поиск
Категории
Больше
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-02-05 13:05:59 0 6Кб
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 23
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-26 04:15:25 0 6Кб
Injili Ya Yesu Kristo
Ubatizo Wa Roho Mtakatifu
Mtu anaposoma kitabu cha Matendo ya Mitume, utendaji wa Roho Mtakatifu katika kanisa la kwanza...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:37:38 0 6Кб
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Joshua 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 49 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:40:06 0 6Кб
SPIRITUAL EDUCATION
PASIPO UTAKATIFU NA AMANI HAIZEKANI KUMUONA MUNGU (EBRANIA 12:14 PART 01:)
PASIPO UTAKATIFU NA AMANI HAIZEKANI KUMUONA MUNGU (EBRANIA 12:14 PART 01:)
От Martin Laizer 2023-10-18 11:55:36 2 9Кб