Je! kuna dhambi kubwa na ndogo?

0
5كيلو بايت

SWALI: Naomba kufahamu Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?


JIBU: Dhambi ni dhambi iwe kubwa au ndogo, zote ni kosa, biblia inasema.

Yakobo 2:10 “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. 11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. “

Unaona hapo? Kwahiyo mtu akitenda dhambi iwe kubwa au ndogo ataadhibiwa. lakini adhabu zitatofautiana huko waendako kulingana na wingi wa makosa, kwasababu Bwana Yesu pia alisema aliyeua kwa upanga atauawa kwa upanga, apandacho mtu ndicho atakachovuna. adhabu ya shetani haiwezi ikawa sawa na adhabu ya mwanadamu. Biblia inaeleza..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, ATAPIGWA SANA. 48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, ATAPIGWA KIDOGO. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi. “

Kwahiyo mapigo yanatofautiana kulingana na matendo ya mtu aliyoyatenda akiwa hapa duniani, ni kama tu vile thawabu zitavyotofautiana kwa mtu na mtu mbinguni kwa jinsi alivyotaabika katika kumtumikia Bwana vivyo hivyo na jehanamu adhabu zitatofautiana kulingana na dhambi mtu alizotenda akiwa ulimwenguni. Na jinsi gani alivyoipuuzia neema ya wokovu.

Hivyo hatupaswi kuipima dhambi kwa namna yoyote, ni kukaa nayo mbali kwasababu iwe ni kubwa au ndogo mshahara wake ni MAUTI, Warumi 6:23.

Dhambi kubwa na ndoto zote zina adhabu ya mauti.

Je! Umempa Yesu maisha yako ndugu yangu? Unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho?. Ukifa leo utakuwa mgeni wa nani, huko uendako?. Tubu sasa mgeukie yeye atakusamehe, na kukupa uzima wa milele.

Mungu akubariki.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
SPIRITUAL EDUCATION
INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA* .
INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA* .
بواسطة Martin Laizer 2023-10-17 20:10:29 7 6كيلو بايت
SPIRITUAL EDUCATION
THE SPIRIT OF TRUTH
John 14:16-17 is written “And I will ask the Father, and He will give you another...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:33:12 0 5كيلو بايت
REVELATION
UFUNUO 12
MAELEZO JUU YA “UFUNUO 12” Ufunuo 12 1 Na ishara kuu ilionekana mbinguni;...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:35:41 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
MWISHO WA DUNIA NI LINI? UNYAKUO NI LINI?
JE UNAJUA NI LINI? NA JE UNAJUA NI KWA NINI WATUMISHI WANATABIRI UONGO KUHUSU MWISHO WA DUNIA?...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:54:05 0 5كيلو بايت
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
GFG
FDF
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-12-31 12:37:18 0 5كيلو بايت