Je! kuna dhambi kubwa na ndogo?

0
5K

SWALI: Naomba kufahamu Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?


JIBU: Dhambi ni dhambi iwe kubwa au ndogo, zote ni kosa, biblia inasema.

Yakobo 2:10 “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. 11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. “

Unaona hapo? Kwahiyo mtu akitenda dhambi iwe kubwa au ndogo ataadhibiwa. lakini adhabu zitatofautiana huko waendako kulingana na wingi wa makosa, kwasababu Bwana Yesu pia alisema aliyeua kwa upanga atauawa kwa upanga, apandacho mtu ndicho atakachovuna. adhabu ya shetani haiwezi ikawa sawa na adhabu ya mwanadamu. Biblia inaeleza..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, ATAPIGWA SANA. 48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, ATAPIGWA KIDOGO. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi. “

Kwahiyo mapigo yanatofautiana kulingana na matendo ya mtu aliyoyatenda akiwa hapa duniani, ni kama tu vile thawabu zitavyotofautiana kwa mtu na mtu mbinguni kwa jinsi alivyotaabika katika kumtumikia Bwana vivyo hivyo na jehanamu adhabu zitatofautiana kulingana na dhambi mtu alizotenda akiwa ulimwenguni. Na jinsi gani alivyoipuuzia neema ya wokovu.

Hivyo hatupaswi kuipima dhambi kwa namna yoyote, ni kukaa nayo mbali kwasababu iwe ni kubwa au ndogo mshahara wake ni MAUTI, Warumi 6:23.

Dhambi kubwa na ndoto zote zina adhabu ya mauti.

Je! Umempa Yesu maisha yako ndugu yangu? Unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho?. Ukifa leo utakuwa mgeni wa nani, huko uendako?. Tubu sasa mgeukie yeye atakusamehe, na kukupa uzima wa milele.

Mungu akubariki.

Cerca
Categorie
Leggi tutto
Injili Ya Yesu Kristo
JIFUNZE KUENENDA KWA ROHO ILI USIMHUZUNISHE ROHO MTAKATIFU
Shalom, hakuna namna mwamini anaweza kuishi maisha ya kumpendeza Mungu hapa duniani bila kuenenda...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:54:38 0 6K
MASWALI & MAJIBU
Kuna Ufufuo Wa Aina Ngapi?
JIBU: Biblia inasema kuna ufufuo wa aina mbili, Ufufuo wa kwanza, umejumuisha wale...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:16:59 0 5K
OTHERS
MUHAMMAD ALIKUWA NA WAKE ZAIDI YA 20
Huu ni MSIBA mkubwa sana. Ifuatayo ni orodha ya wake wa Muhammad iliyoandaliwa na mwanazuoni wa...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:48:32 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Hekima yao ikapate kuwa ubatili na maarifa yao yawe ujinga!
2Samuel 15:30-31 “Daudi akapanda akishika njia ya kuupandia mlima wa Mizeituni, akilia...
By GOSPEL PREACHER 2022-04-01 09:26:31 4 6K
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 6
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-01 22:06:14 0 5K