YESU ATAKUPONYA.

0
5K

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi,

“Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu. Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.” Luka 5:19-20

Najaribu kukutia moyo kuhusu ugonjwa wa mwili unaopitia sasa,kwamba usikate tamaa kwa maana yupo Mungu aponyaye. Maandiko yanatueleza ile kweli halisi kuhusu uponyaji uliopo ndani ya Yesu. Bila shaka mgonjwa huyu alichukuliwa na watu wanne yeye akiwa hoi kitandani. Ashukuriwe Mungu hawa ndugu wanne walikuwa wapi kwa kumpeleka mgonjwa wao ili apone. Namna tu ya kujua sehemu sahihi ya uponyaji wako nalo ni neno kubwa sana.

Kwa sababu wapo wagonjwa wengi ambao wamekata kauli lakini wale wanaossimamia hawajui mahali sahihi pa kumpeleka,na ndio maana wapo wagonjwa waliopelekwa kwa waganga wa tungulisi kama walikuwa wanapenda au kutaka lakini walijikuta wako kwa waganga wa tunguli,kwa sababu waliomchukua hana maarifa sahihi. Bila shaka mgonjwa hakuwa na maazi ya wapi apelekwe na wapi asipelekwe,labda alikata kauli au labda hana sauti. Lakini tunawapongeza wale waliomchukua na kumpeleka kwa mponyaji,Yesu Kristo wa Nazareti. Yesu huyo huyo yupo hata sasa,ukiamini tu,utapona.

Huyu mgonjwa labda alikuwa wala aamini habari za Yesu,nalo ni jambo la kushangaza. Lakini Yesu alimponya pale alipoiona imani yao wale waliomchukua hata kupangua matofali ya dari / paa la watu. Hawa ndugu walikuwa na akili maana hawakuvunja paa la watu,bali walipangua kwa utaratibu ili wasipate gharama ya kulipa paa. Lakini Yesu alipowaona,aliona imani yao,hii ina maana “imani ” ni muhimu sana ikiwa kama unahitaji kuapona. Ni lazima uamini kwanza,tena na ni vyema ili upokee uponyaji kikamilifu. hata leo ukiomba kwa imani,tegemea kupona hata kama sio leo basi kesho utapona tu. Usife moyo,usikate tamaa yupo Mungu aponyaye hata sasa.

Search
Categories
Read More
JOSHUA
Book of Joshua Explained
Title: This is the first of the 12 historical books, and it gained its name from the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:10:22 0 6K
MASWALI & MAJIBU
Je! Inawezekana mtu akawa anafanya miujiza na bado asinyakuliwe?
SWALI: Naomba kuelewa kwanini mtu atoe pepo, aombee wagonjwa wapone, asikie sauti ya Mungu...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-12 23:16:05 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
Looking at the false doctrine of ‘once saved, always saved’
The false doctrine of “once saved, always saved” teaches that it is not possible for...
By PROSPER HABONA 2022-01-16 14:43:41 0 5K
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:40:06 0 5K
OTHERS
JE DHAMBI NI NINI?
Biblia inatueleza kuhusu hii dhambi kuwa ni kitu gani. Inafafanua kuwa dhambi ni “uasi au...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:16:57 0 5K