YESU ATAKUPONYA.

0
5K

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi,

“Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu. Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.” Luka 5:19-20

Najaribu kukutia moyo kuhusu ugonjwa wa mwili unaopitia sasa,kwamba usikate tamaa kwa maana yupo Mungu aponyaye. Maandiko yanatueleza ile kweli halisi kuhusu uponyaji uliopo ndani ya Yesu. Bila shaka mgonjwa huyu alichukuliwa na watu wanne yeye akiwa hoi kitandani. Ashukuriwe Mungu hawa ndugu wanne walikuwa wapi kwa kumpeleka mgonjwa wao ili apone. Namna tu ya kujua sehemu sahihi ya uponyaji wako nalo ni neno kubwa sana.

Kwa sababu wapo wagonjwa wengi ambao wamekata kauli lakini wale wanaossimamia hawajui mahali sahihi pa kumpeleka,na ndio maana wapo wagonjwa waliopelekwa kwa waganga wa tungulisi kama walikuwa wanapenda au kutaka lakini walijikuta wako kwa waganga wa tunguli,kwa sababu waliomchukua hana maarifa sahihi. Bila shaka mgonjwa hakuwa na maazi ya wapi apelekwe na wapi asipelekwe,labda alikata kauli au labda hana sauti. Lakini tunawapongeza wale waliomchukua na kumpeleka kwa mponyaji,Yesu Kristo wa Nazareti. Yesu huyo huyo yupo hata sasa,ukiamini tu,utapona.

Huyu mgonjwa labda alikuwa wala aamini habari za Yesu,nalo ni jambo la kushangaza. Lakini Yesu alimponya pale alipoiona imani yao wale waliomchukua hata kupangua matofali ya dari / paa la watu. Hawa ndugu walikuwa na akili maana hawakuvunja paa la watu,bali walipangua kwa utaratibu ili wasipate gharama ya kulipa paa. Lakini Yesu alipowaona,aliona imani yao,hii ina maana “imani ” ni muhimu sana ikiwa kama unahitaji kuapona. Ni lazima uamini kwanza,tena na ni vyema ili upokee uponyaji kikamilifu. hata leo ukiomba kwa imani,tegemea kupona hata kama sio leo basi kesho utapona tu. Usife moyo,usikate tamaa yupo Mungu aponyaye hata sasa.

Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
URAFIKI KIBIBLIA
JE, MAAMUZI YA NANI ATAKUWA MWENZI WAKO WA MAISHA NI YA MUNGU AU YA KWAKO?
Mithali 19:14 “Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; bali mke mwenye busara mtu...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:28:14 0 6K
OTHERS
Waislam Wauliza Wakristo
  Swali la 1: Kwa nini mnaliamini Agano la Kale? Jibu: Maandiko na elimukale...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:40:11 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
MBWEHA WADOGO WAIHARIBUO MIZABIBU
Wimbo uliobora 2:15 “Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana...
By GOSPEL PREACHER 2022-03-31 14:34:48 0 8K
OTHERS
JE, ISA NI JINA SAHIHI LA YESU WA BIBLIA?
Katika somo letu hili tutajifunza kuhusu jina sahihi la Yesu/Yashua na tafsiri yake katika...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:28:15 0 5K
HOLY BIBLE
Jesus' Two Natures: God and Man
Jesus is the most important person who has ever lived since he is the savior, God in human...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:45:51 0 5K