YESU ATAKUPONYA.

0
4KB

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi,

“Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu. Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.” Luka 5:19-20

Najaribu kukutia moyo kuhusu ugonjwa wa mwili unaopitia sasa,kwamba usikate tamaa kwa maana yupo Mungu aponyaye. Maandiko yanatueleza ile kweli halisi kuhusu uponyaji uliopo ndani ya Yesu. Bila shaka mgonjwa huyu alichukuliwa na watu wanne yeye akiwa hoi kitandani. Ashukuriwe Mungu hawa ndugu wanne walikuwa wapi kwa kumpeleka mgonjwa wao ili apone. Namna tu ya kujua sehemu sahihi ya uponyaji wako nalo ni neno kubwa sana.

Kwa sababu wapo wagonjwa wengi ambao wamekata kauli lakini wale wanaossimamia hawajui mahali sahihi pa kumpeleka,na ndio maana wapo wagonjwa waliopelekwa kwa waganga wa tungulisi kama walikuwa wanapenda au kutaka lakini walijikuta wako kwa waganga wa tunguli,kwa sababu waliomchukua hana maarifa sahihi. Bila shaka mgonjwa hakuwa na maazi ya wapi apelekwe na wapi asipelekwe,labda alikata kauli au labda hana sauti. Lakini tunawapongeza wale waliomchukua na kumpeleka kwa mponyaji,Yesu Kristo wa Nazareti. Yesu huyo huyo yupo hata sasa,ukiamini tu,utapona.

Huyu mgonjwa labda alikuwa wala aamini habari za Yesu,nalo ni jambo la kushangaza. Lakini Yesu alimponya pale alipoiona imani yao wale waliomchukua hata kupangua matofali ya dari / paa la watu. Hawa ndugu walikuwa na akili maana hawakuvunja paa la watu,bali walipangua kwa utaratibu ili wasipate gharama ya kulipa paa. Lakini Yesu alipowaona,aliona imani yao,hii ina maana “imani ” ni muhimu sana ikiwa kama unahitaji kuapona. Ni lazima uamini kwanza,tena na ni vyema ili upokee uponyaji kikamilifu. hata leo ukiomba kwa imani,tegemea kupona hata kama sio leo basi kesho utapona tu. Usife moyo,usikate tamaa yupo Mungu aponyaye hata sasa.

Rechercher
Catégories
Lire la suite
FORM 2
FORM 2
List of all subjects for the form 2 class AGRICULTURE BASIC MATHEMETICS BIOLOGY BOOK-KEEPING...
Par PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:23:39 0 5KB
BACHELOR
BACHELOR
List of all subjects for the students who are taking bachelor courses.
Par PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:55:07 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
MBINGUNI, PEPONI, KUZIMU NA JEHANNAM NI WAPI?
Mpendwa mmoja aliniuliza maswali yafuatayo ambayo nimeona ni muhimu niyajibu kama Makala fupi kwa...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-25 11:56:58 0 6KB
Religion
UFAHAMU KUHUSU DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU
VIPENGELE VYA SOMO(1). NI MAANA YA KUKUFURU?(2). DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU IKOJEE?(3)....
Par GOSPEL PREACHER 2021-08-24 12:44:21 4 8KB
SPIRITUAL EDUCATION
MAVAZI YA KIKAHABA NI MACHUKIZO KWA BWANA MUNGU WAKO.
MAVAZI YA KIKAHABA NI MACHUKIZO KWA BWANA MUNGU WAKO 
Par Martin Laizer 2023-10-07 09:24:32 1 14KB