YESU ATAKUPONYA.

0
4K

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi,

“Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu. Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.” Luka 5:19-20

Najaribu kukutia moyo kuhusu ugonjwa wa mwili unaopitia sasa,kwamba usikate tamaa kwa maana yupo Mungu aponyaye. Maandiko yanatueleza ile kweli halisi kuhusu uponyaji uliopo ndani ya Yesu. Bila shaka mgonjwa huyu alichukuliwa na watu wanne yeye akiwa hoi kitandani. Ashukuriwe Mungu hawa ndugu wanne walikuwa wapi kwa kumpeleka mgonjwa wao ili apone. Namna tu ya kujua sehemu sahihi ya uponyaji wako nalo ni neno kubwa sana.

Kwa sababu wapo wagonjwa wengi ambao wamekata kauli lakini wale wanaossimamia hawajui mahali sahihi pa kumpeleka,na ndio maana wapo wagonjwa waliopelekwa kwa waganga wa tungulisi kama walikuwa wanapenda au kutaka lakini walijikuta wako kwa waganga wa tunguli,kwa sababu waliomchukua hana maarifa sahihi. Bila shaka mgonjwa hakuwa na maazi ya wapi apelekwe na wapi asipelekwe,labda alikata kauli au labda hana sauti. Lakini tunawapongeza wale waliomchukua na kumpeleka kwa mponyaji,Yesu Kristo wa Nazareti. Yesu huyo huyo yupo hata sasa,ukiamini tu,utapona.

Huyu mgonjwa labda alikuwa wala aamini habari za Yesu,nalo ni jambo la kushangaza. Lakini Yesu alimponya pale alipoiona imani yao wale waliomchukua hata kupangua matofali ya dari / paa la watu. Hawa ndugu walikuwa na akili maana hawakuvunja paa la watu,bali walipangua kwa utaratibu ili wasipate gharama ya kulipa paa. Lakini Yesu alipowaona,aliona imani yao,hii ina maana “imani ” ni muhimu sana ikiwa kama unahitaji kuapona. Ni lazima uamini kwanza,tena na ni vyema ili upokee uponyaji kikamilifu. hata leo ukiomba kwa imani,tegemea kupona hata kama sio leo basi kesho utapona tu. Usife moyo,usikate tamaa yupo Mungu aponyaye hata sasa.

Zoeken
Categorieën
Read More
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 11
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-22 11:28:51 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
JINSI SADAKA ZA WANA WA MUNGU ZINAVYOIBIWA WAKIFIKIRI WANAMTOLEA MUNGU NA KUMBE WAMEIBIWA PESA ZAO NA WATUMISHI.
BWANA YESU ASIFIWE. YESU WA NAZARETI aliye hai, tena anawapenda watu wote wabarikiwe kupitia njia...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:37:43 0 5K
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
The difference between an invoice and a bill
  ‘Invoice’ and ‘bill’ are two terms that are often...
By PROSHABO ACCOUNTING 2022-02-02 03:32:07 0 7K
NDOA KIBIBLIA
MWANAUME: KAA NA MKE WAKO KWA AKILI
KWELI KUU: Mwanaume mwenye akili akishindwa kukaa na mke wake ni kwa sababu amekosa akili.1Petro...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-07 22:20:56 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
KUBOMOA MADHABAHU ZA SHETANI
Madhabahu ni nini? Ni daraja la kuunganisha katika ya ulimwengu wa roho wa Mungu au shetani. Kuna...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-19 07:26:43 0 7K