YESU ATAKUPONYA.

0
5KB

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi,

“Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu. Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.” Luka 5:19-20

Najaribu kukutia moyo kuhusu ugonjwa wa mwili unaopitia sasa,kwamba usikate tamaa kwa maana yupo Mungu aponyaye. Maandiko yanatueleza ile kweli halisi kuhusu uponyaji uliopo ndani ya Yesu. Bila shaka mgonjwa huyu alichukuliwa na watu wanne yeye akiwa hoi kitandani. Ashukuriwe Mungu hawa ndugu wanne walikuwa wapi kwa kumpeleka mgonjwa wao ili apone. Namna tu ya kujua sehemu sahihi ya uponyaji wako nalo ni neno kubwa sana.

Kwa sababu wapo wagonjwa wengi ambao wamekata kauli lakini wale wanaossimamia hawajui mahali sahihi pa kumpeleka,na ndio maana wapo wagonjwa waliopelekwa kwa waganga wa tungulisi kama walikuwa wanapenda au kutaka lakini walijikuta wako kwa waganga wa tunguli,kwa sababu waliomchukua hana maarifa sahihi. Bila shaka mgonjwa hakuwa na maazi ya wapi apelekwe na wapi asipelekwe,labda alikata kauli au labda hana sauti. Lakini tunawapongeza wale waliomchukua na kumpeleka kwa mponyaji,Yesu Kristo wa Nazareti. Yesu huyo huyo yupo hata sasa,ukiamini tu,utapona.

Huyu mgonjwa labda alikuwa wala aamini habari za Yesu,nalo ni jambo la kushangaza. Lakini Yesu alimponya pale alipoiona imani yao wale waliomchukua hata kupangua matofali ya dari / paa la watu. Hawa ndugu walikuwa na akili maana hawakuvunja paa la watu,bali walipangua kwa utaratibu ili wasipate gharama ya kulipa paa. Lakini Yesu alipowaona,aliona imani yao,hii ina maana “imani ” ni muhimu sana ikiwa kama unahitaji kuapona. Ni lazima uamini kwanza,tena na ni vyema ili upokee uponyaji kikamilifu. hata leo ukiomba kwa imani,tegemea kupona hata kama sio leo basi kesho utapona tu. Usife moyo,usikate tamaa yupo Mungu aponyaye hata sasa.

Suche
Kategorien
Mehr lesen
MASWALI & MAJIBU
Je! Wayahudi Wote Wataokolewa Kulingana Na Warumi 11:26?
SWALI: Je! Wayahudi wote wataokolewa? maana biblia inasema katika; Warumi 11:25...
Von GOSPEL PREACHER 2022-06-13 00:22:40 0 5KB
DANIEL
DANELI 6
Jina KUU la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe. Ndugu mpenzi karibu tujifunze Neno la Mungu na...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-05 23:52:47 0 7KB
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 16
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 19 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-05-20 11:58:21 0 8KB
2 KINGS
Verse by verse explanation of 2 Kings 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-03-19 19:48:57 0 5KB
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 27
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 43 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:40:12 0 6KB