Je! Mkristo anaweza pagagwa na Mapepo?

0
5K
Bibilia kwa ukamilifu haitaji kama Mkristo anaweza shikwa na pepo. Ingagwa, kwa vile Mkristo amejazwa na Roho Mtakatifu (Warumi 8:9-11; 1 Wakorintho 3:16; 6:19), inaweza ooneka kinyume kwamba Roho Mtakatifu anaweza kumuruhus pepo kushika mtu ambaye Roho Mtakatifu anakaa ndani yake. Hii mara nyingine ni jambo la kutatanisha; ingawa, tunaamini sana kuwa Mkristo hawezi shikwa na pepo. Tunaamini kuwa kuna tofauti kubwa kati ya kushikwa na pepo na kukandamizwa na pepo au kushawishika na pepo. Kupagagwa na pepo yahuzisha,pepo kuwa na uhusika wa Karibu au kuongoza mawazo yako/mafikirio yako/matendo ya mtu (Luka 4:33-35; 8:27-33; Mathayo 17:14-18). Kukandamizwa na pepo au kushawishiwa na pepo inahuzisha pepo kumkabili mtu kiroho na kumtia moyo kwa matendo ya dhambi (1 Petero 5:8-0; Yakobo 4:7). Tambua kwamba kurasa zote za Agano Jipya zashugulikia vita vya kiroho, kamwe hatwambiwi kutoa pepo kutoka kwa mkristo (Waefeso 6:10-18). Wakristo wameambiwa kumtoroka shetani (1 Petero 5:8-9; Yakobo 4:7), si kutoa mapepo.

 
Ni jambo lisilofikirika kuwa Mungu anaweza kumruhus mwanawe, ambaye alimununua kwa dhamani, kwa damu ya Yesu Kristo (1 Petero 1:18-19), na kufanywa viumbe vipya (2 Wakorintho 5:17), kupagagwa na kutawaliwa na mapepo. Naam, mkristo twafanya vita na shetani na mapepo yake, lakini si kutoka ndani yetu. Mtume Yohana anasema, “Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mtungu; ninyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko aliye katika dunia” (1 Yohana 4:4). Ni nani aliye ndani yetu? Roho Mtakatifu. Ni nani aliye katika dunia? Ni shetani na mapepo yake. Kwa hivyo, mkristo ameushinda ulimwengu wa mapepo, na hali ya kupagagwa na pepo halitafanywa kuwa la kibilia.
Buscar
Categorías
Read More
Religion
Sadaka inayomgusa Mungu
Nianze kwa kuwashukuru na kuwapongeza wasomaji wa makala hii, najua kuna faida nyingi za kiroho,...
By GOSPEL PREACHER 2021-08-25 09:39:38 0 9K
DARASA LA 4
DARASA LA 4
Orodha ya masomo yote ya darasa la 4
By PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:15:37 0 5K
MASWALI & MAJIBU
Je! kuna dhambi kubwa na ndogo?
SWALI: Naomba kufahamu Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 00:12:35 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
MATENDO YA HURUMA.
Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi…  Tunaposema “ matendo ya...
By GOSPEL PREACHER 2022-03-30 04:58:16 0 6K
OTHERS
MUHAMMAD ALIKUWA NA DHAMBI KUBWA KIASI CHA KUOMBA MSAMAHA MARA MIA KWA SIKU
Dhambi kubwa Katika "Sahih Muslim, Kitabu 35, 6522 Idadi" inasema kwamba Muhammad alikuwa...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:14:15 0 5K