Je! Mkristo anaweza pagagwa na Mapepo?

0
5K
Bibilia kwa ukamilifu haitaji kama Mkristo anaweza shikwa na pepo. Ingagwa, kwa vile Mkristo amejazwa na Roho Mtakatifu (Warumi 8:9-11; 1 Wakorintho 3:16; 6:19), inaweza ooneka kinyume kwamba Roho Mtakatifu anaweza kumuruhus pepo kushika mtu ambaye Roho Mtakatifu anakaa ndani yake. Hii mara nyingine ni jambo la kutatanisha; ingawa, tunaamini sana kuwa Mkristo hawezi shikwa na pepo. Tunaamini kuwa kuna tofauti kubwa kati ya kushikwa na pepo na kukandamizwa na pepo au kushawishika na pepo. Kupagagwa na pepo yahuzisha,pepo kuwa na uhusika wa Karibu au kuongoza mawazo yako/mafikirio yako/matendo ya mtu (Luka 4:33-35; 8:27-33; Mathayo 17:14-18). Kukandamizwa na pepo au kushawishiwa na pepo inahuzisha pepo kumkabili mtu kiroho na kumtia moyo kwa matendo ya dhambi (1 Petero 5:8-0; Yakobo 4:7). Tambua kwamba kurasa zote za Agano Jipya zashugulikia vita vya kiroho, kamwe hatwambiwi kutoa pepo kutoka kwa mkristo (Waefeso 6:10-18). Wakristo wameambiwa kumtoroka shetani (1 Petero 5:8-9; Yakobo 4:7), si kutoa mapepo.

 
Ni jambo lisilofikirika kuwa Mungu anaweza kumruhus mwanawe, ambaye alimununua kwa dhamani, kwa damu ya Yesu Kristo (1 Petero 1:18-19), na kufanywa viumbe vipya (2 Wakorintho 5:17), kupagagwa na kutawaliwa na mapepo. Naam, mkristo twafanya vita na shetani na mapepo yake, lakini si kutoka ndani yetu. Mtume Yohana anasema, “Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mtungu; ninyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko aliye katika dunia” (1 Yohana 4:4). Ni nani aliye ndani yetu? Roho Mtakatifu. Ni nani aliye katika dunia? Ni shetani na mapepo yake. Kwa hivyo, mkristo ameushinda ulimwengu wa mapepo, na hali ya kupagagwa na pepo halitafanywa kuwa la kibilia.
Cerca
Categorie
Leggi tutto
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 23 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 08:27:26 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
ENYI WANAWAKE MSINILILIE MIMI
Kwa nini Yesu aliwaambia akinamama jililieni nafsi zenu na watoto wenu ?Luka 23:27-28 “Na...
By GOSPEL PREACHER 2021-12-16 12:14:49 0 5K
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 32 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-03-20 04:43:04 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
YAFAHAMU MAFUNDISHO YA UONGO
(basi roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani wakiyasikiliza...
By GOSPEL PREACHER 2021-12-22 01:41:05 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Je umeshapata Zawadi ya Uzima wa milele?
Bibilia inaonyesha njia ya wazi ya uzimani.Mwanzo ni sharti tutambue yakwamba tumetenda dhambi...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:42:08 0 6K