Je! Mkristo anaweza pagagwa na Mapepo?

0
5K
Bibilia kwa ukamilifu haitaji kama Mkristo anaweza shikwa na pepo. Ingagwa, kwa vile Mkristo amejazwa na Roho Mtakatifu (Warumi 8:9-11; 1 Wakorintho 3:16; 6:19), inaweza ooneka kinyume kwamba Roho Mtakatifu anaweza kumuruhus pepo kushika mtu ambaye Roho Mtakatifu anakaa ndani yake. Hii mara nyingine ni jambo la kutatanisha; ingawa, tunaamini sana kuwa Mkristo hawezi shikwa na pepo. Tunaamini kuwa kuna tofauti kubwa kati ya kushikwa na pepo na kukandamizwa na pepo au kushawishika na pepo. Kupagagwa na pepo yahuzisha,pepo kuwa na uhusika wa Karibu au kuongoza mawazo yako/mafikirio yako/matendo ya mtu (Luka 4:33-35; 8:27-33; Mathayo 17:14-18). Kukandamizwa na pepo au kushawishiwa na pepo inahuzisha pepo kumkabili mtu kiroho na kumtia moyo kwa matendo ya dhambi (1 Petero 5:8-0; Yakobo 4:7). Tambua kwamba kurasa zote za Agano Jipya zashugulikia vita vya kiroho, kamwe hatwambiwi kutoa pepo kutoka kwa mkristo (Waefeso 6:10-18). Wakristo wameambiwa kumtoroka shetani (1 Petero 5:8-9; Yakobo 4:7), si kutoa mapepo.

 
Ni jambo lisilofikirika kuwa Mungu anaweza kumruhus mwanawe, ambaye alimununua kwa dhamani, kwa damu ya Yesu Kristo (1 Petero 1:18-19), na kufanywa viumbe vipya (2 Wakorintho 5:17), kupagagwa na kutawaliwa na mapepo. Naam, mkristo twafanya vita na shetani na mapepo yake, lakini si kutoka ndani yetu. Mtume Yohana anasema, “Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mtungu; ninyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko aliye katika dunia” (1 Yohana 4:4). Ni nani aliye ndani yetu? Roho Mtakatifu. Ni nani aliye katika dunia? Ni shetani na mapepo yake. Kwa hivyo, mkristo ameushinda ulimwengu wa mapepo, na hali ya kupagagwa na pepo halitafanywa kuwa la kibilia.
Cerca
Categorie
Leggi tutto
URAFIKI KIBIBLIA
JINSI YA KUMJUA MWENZI WAKO ALIYEKUSUDIWA NA MUNGU
Leo napenda tuangalie mambo yatakayokufanya umjue mwenzi wako wa ndoa uliyekusudiwa na Mungu....
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 13:01:29 0 7K
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 136 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-22 11:33:32 0 6K
NEHEMIAH
Verse by verse explanation of Nehemiah 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-02 12:36:58 0 6K
MAHUSIANO KIBIBLIA
KANUNI YA MUDA KATIKA MAHUSIANO
Muda hupima upendo wangu kwako.Kama kweli nakupenda, nita tumia kiasi kikubwa cha Muda wangu kwa...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 15:03:16 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
MWISHO WA DUNIA NI LINI? UNYAKUO NI LINI?
JE UNAJUA NI LINI? NA JE UNAJUA NI KWA NINI WATUMISHI WANATABIRI UONGO KUHUSU MWISHO WA DUNIA?...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:54:05 0 5K