Je! Mkristo anaweza pagagwa na Mapepo?

0
5KB
Bibilia kwa ukamilifu haitaji kama Mkristo anaweza shikwa na pepo. Ingagwa, kwa vile Mkristo amejazwa na Roho Mtakatifu (Warumi 8:9-11; 1 Wakorintho 3:16; 6:19), inaweza ooneka kinyume kwamba Roho Mtakatifu anaweza kumuruhus pepo kushika mtu ambaye Roho Mtakatifu anakaa ndani yake. Hii mara nyingine ni jambo la kutatanisha; ingawa, tunaamini sana kuwa Mkristo hawezi shikwa na pepo. Tunaamini kuwa kuna tofauti kubwa kati ya kushikwa na pepo na kukandamizwa na pepo au kushawishika na pepo. Kupagagwa na pepo yahuzisha,pepo kuwa na uhusika wa Karibu au kuongoza mawazo yako/mafikirio yako/matendo ya mtu (Luka 4:33-35; 8:27-33; Mathayo 17:14-18). Kukandamizwa na pepo au kushawishiwa na pepo inahuzisha pepo kumkabili mtu kiroho na kumtia moyo kwa matendo ya dhambi (1 Petero 5:8-0; Yakobo 4:7). Tambua kwamba kurasa zote za Agano Jipya zashugulikia vita vya kiroho, kamwe hatwambiwi kutoa pepo kutoka kwa mkristo (Waefeso 6:10-18). Wakristo wameambiwa kumtoroka shetani (1 Petero 5:8-9; Yakobo 4:7), si kutoa mapepo.

 
Ni jambo lisilofikirika kuwa Mungu anaweza kumruhus mwanawe, ambaye alimununua kwa dhamani, kwa damu ya Yesu Kristo (1 Petero 1:18-19), na kufanywa viumbe vipya (2 Wakorintho 5:17), kupagagwa na kutawaliwa na mapepo. Naam, mkristo twafanya vita na shetani na mapepo yake, lakini si kutoka ndani yetu. Mtume Yohana anasema, “Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mtungu; ninyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko aliye katika dunia” (1 Yohana 4:4). Ni nani aliye ndani yetu? Roho Mtakatifu. Ni nani aliye katika dunia? Ni shetani na mapepo yake. Kwa hivyo, mkristo ameushinda ulimwengu wa mapepo, na hali ya kupagagwa na pepo halitafanywa kuwa la kibilia.
Pesquisar
Categorias
Leia mais
Injili Ya Yesu Kristo
MASWALI YA KITABU CHA MWANZO
MASWALI YA KITABU CHA MWANZO KWA WATOTO Nani alimwuzia mwenzake haki ya...
Por PROSPER HABONA 2024-01-07 04:56:40 0 4KB
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 43 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-01 10:35:25 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
YESU NI MWANA WA MUNGU
Je, ina maana gani Yesu kuwa Mwana wa Mungu    Ndugu Msomaji, Yesu si Mwana wa Mungu...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:24:13 0 5KB
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 54 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-03-20 04:30:57 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
MAFUNDISHO YA MASHETANI
1 Timotheo 4 : 1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine...
Por GOSPEL PREACHER 2022-06-04 16:00:49 0 6KB