Ni kwa nini uzao wa ubikira ni wa maana?

0
5Кб
 Funzo la uzao wa ubikira ni la maana sana (Isaya 7:14 Mathayo 1:23; Luka 1:27,34). Kwanza, hebu tuangazie vile bibilia inavyo lieleza swala la uzao wa ubikira. Kulingana na swali la Mariamu, “Litakuwaje neno hili?” (Luka 1:34), Gabrieli anasema, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu” (Luka 1:35). Malaika alimtia moyo Zekaria isiwe na hofu mchukue Mariamu kama mke wako kwa maneno haya: “mimba aliyoibeba ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu” (Mathayo 1:18). Wagalatia 4:4 pia yafunza juu ya uzao wa ubikira “Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke.”
 
Kutoka kwa ukurasa huu, ni kweli kwamba kuzaliwa kwa Yesu kulikuwa kwa Roho Mtakatifu uliofanya kazi ndani ya Mariamu. Roho usio na mwili na mwili (tumbo ya Mariamu) vyote viliusika. Mariamu hangeweza kujitia mimba, kwa hali hiyo alitumika kama “chombo” ni Mungu pekee angeweza kutenda muujiza wa mwili na kuchukua ule wa mwanadamu.
 
Kukataa upatanisho wa Mariamu na Yesu itamaanisha kwamba Yesu hakuwa binadamu kabisa. Maandiko yafunza kwamba Yesu alikuwa binadamu, mwili kama wetu. Huu aliupokea kutoka kwa Mariamu. Kwa wakati huo, kikamilifu Yesu alikua Mungu, akiwa na mwili wa milele usio na mawaa (Yohana 1:14; 1Timotheo 3:16; Waebrania 2:14-17.)
 
Yesu hakuzaliwa kwa dhambi; hiyo ni kusema hakuwa na hali ya dhambi (Waebrania 7:26). Itaonekana kuwa hali ya dhambi itapitishwa kutoka kizazi hadi kizazi kingine kupitia kwa baba (Warumi 5:12, 17, 19). Uzao wa ubikira wa Yesu haukufuata hali ile ya kupitisha dhambi kutoka kizazi hadi kizazi na kumruhusu Mungu aishiye milele kuwa mwanadamu kamili.
Поиск
Категории
Больше
JUDGES
Verse by verse explanation of Judges 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 41 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-25 10:49:09 0 6Кб
MASWALI & MAJIBU
Je! Mtu Aliyeokoka Anaruhusiwa Kumiliki Lodge Ambayo Ina Bar Ndani Yake?
Swali linaendelea….na kutoa fungu la kumi kwa kupitia hiyo?,kwa mfano mimi nina rafiki...
От GOSPEL PREACHER 2022-06-13 09:17:15 0 7Кб
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 14
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:06:45 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
JIFUNZE KUMILIKI MAJIBU YA MAOMBI YAKO
Yoshua 13:1-7 Utangulizi, Katika dunia ya leo  watu wengi sana wamekuwa wakitumia muda wao...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:42:34 0 6Кб
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 23 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-03-20 05:07:14 0 6Кб