Ni kwa nini uzao wa ubikira ni wa maana?

0
5كيلو بايت
 Funzo la uzao wa ubikira ni la maana sana (Isaya 7:14 Mathayo 1:23; Luka 1:27,34). Kwanza, hebu tuangazie vile bibilia inavyo lieleza swala la uzao wa ubikira. Kulingana na swali la Mariamu, “Litakuwaje neno hili?” (Luka 1:34), Gabrieli anasema, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu” (Luka 1:35). Malaika alimtia moyo Zekaria isiwe na hofu mchukue Mariamu kama mke wako kwa maneno haya: “mimba aliyoibeba ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu” (Mathayo 1:18). Wagalatia 4:4 pia yafunza juu ya uzao wa ubikira “Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke.”
 
Kutoka kwa ukurasa huu, ni kweli kwamba kuzaliwa kwa Yesu kulikuwa kwa Roho Mtakatifu uliofanya kazi ndani ya Mariamu. Roho usio na mwili na mwili (tumbo ya Mariamu) vyote viliusika. Mariamu hangeweza kujitia mimba, kwa hali hiyo alitumika kama “chombo” ni Mungu pekee angeweza kutenda muujiza wa mwili na kuchukua ule wa mwanadamu.
 
Kukataa upatanisho wa Mariamu na Yesu itamaanisha kwamba Yesu hakuwa binadamu kabisa. Maandiko yafunza kwamba Yesu alikuwa binadamu, mwili kama wetu. Huu aliupokea kutoka kwa Mariamu. Kwa wakati huo, kikamilifu Yesu alikua Mungu, akiwa na mwili wa milele usio na mawaa (Yohana 1:14; 1Timotheo 3:16; Waebrania 2:14-17.)
 
Yesu hakuzaliwa kwa dhambi; hiyo ni kusema hakuwa na hali ya dhambi (Waebrania 7:26). Itaonekana kuwa hali ya dhambi itapitishwa kutoka kizazi hadi kizazi kingine kupitia kwa baba (Warumi 5:12, 17, 19). Uzao wa ubikira wa Yesu haukufuata hali ile ya kupitisha dhambi kutoka kizazi hadi kizazi na kumruhusu Mungu aishiye milele kuwa mwanadamu kamili.
البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 58 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-22 11:23:54 0 5كيلو بايت
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 34
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-21 08:57:48 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
NAMNA YA KUMWITA,KWENDA NA KUMUOMBA MUNGU ILI AKUSIKILIZE.
Yeremia 29:12 “Nanyi mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami nitawasikiliza”....
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:21:47 0 5كيلو بايت
SPIRITUAL EDUCATION
The Holy Spirit In The Life Of Christ
In Luke 1:35 the angel Gabriel announces to Mary, “The Holy Spirit will come upon...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:33:40 0 6كيلو بايت
OTHERS
LaTeX/Mathematics
< LaTeX Jump to navigationJump to search LaTeX One of the greatest...
بواسطة PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2022-10-24 14:04:03 0 9كيلو بايت