Ni kwa nini uzao wa ubikira ni wa maana?

0
5KB
 Funzo la uzao wa ubikira ni la maana sana (Isaya 7:14 Mathayo 1:23; Luka 1:27,34). Kwanza, hebu tuangazie vile bibilia inavyo lieleza swala la uzao wa ubikira. Kulingana na swali la Mariamu, “Litakuwaje neno hili?” (Luka 1:34), Gabrieli anasema, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu” (Luka 1:35). Malaika alimtia moyo Zekaria isiwe na hofu mchukue Mariamu kama mke wako kwa maneno haya: “mimba aliyoibeba ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu” (Mathayo 1:18). Wagalatia 4:4 pia yafunza juu ya uzao wa ubikira “Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke.”
 
Kutoka kwa ukurasa huu, ni kweli kwamba kuzaliwa kwa Yesu kulikuwa kwa Roho Mtakatifu uliofanya kazi ndani ya Mariamu. Roho usio na mwili na mwili (tumbo ya Mariamu) vyote viliusika. Mariamu hangeweza kujitia mimba, kwa hali hiyo alitumika kama “chombo” ni Mungu pekee angeweza kutenda muujiza wa mwili na kuchukua ule wa mwanadamu.
 
Kukataa upatanisho wa Mariamu na Yesu itamaanisha kwamba Yesu hakuwa binadamu kabisa. Maandiko yafunza kwamba Yesu alikuwa binadamu, mwili kama wetu. Huu aliupokea kutoka kwa Mariamu. Kwa wakati huo, kikamilifu Yesu alikua Mungu, akiwa na mwili wa milele usio na mawaa (Yohana 1:14; 1Timotheo 3:16; Waebrania 2:14-17.)
 
Yesu hakuzaliwa kwa dhambi; hiyo ni kusema hakuwa na hali ya dhambi (Waebrania 7:26). Itaonekana kuwa hali ya dhambi itapitishwa kutoka kizazi hadi kizazi kingine kupitia kwa baba (Warumi 5:12, 17, 19). Uzao wa ubikira wa Yesu haukufuata hali ile ya kupitisha dhambi kutoka kizazi hadi kizazi na kumruhusu Mungu aishiye milele kuwa mwanadamu kamili.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 30
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 48 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-21 06:56:28 0 5KB
JOB
Verse by verse explanation of Job 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:25:37 0 5KB
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 1
o GENESIS 1   GENESIS 2   GENESIS 3   GENESIS 4   GENESIS 5   GENESIS 6...
Par GOSPEL PREACHER 2021-08-25 14:33:52 0 5KB
OTHERS
NIFANYE NINI ILI KUSHINDA TAMAA ZA MWILI?
JE, NINAWEZA KUISHINDA DHAMBI? Sasa je, tunaweza kweli kuishi humu duniani bila dhambi?  ...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:18:48 0 6KB
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 21
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-02-05 16:01:03 0 6KB