JINSI YA KUISHINDA DHAMBI JUMLA

0
5K
  1. Kubali Kwamba Umeitenda Hiyo Dhambi, Na Usijaribu Kutafuta ANDIKO LA KUJIHAMI, Au MTU WA KUMSINGIZIA..."AFICHAYE DHAMBI ZAKE HATAFANIKIWA, BALI AZIUNGAMAYE NA KUZIACHA, ATAPATA REHEMA"(Mithali 28:13).
  2. Ungama Dhambi Hiyo Kwa Lengo La Kutengeneza Na Mungu..."DHAMBI ZENU ZIMEWAFARAKANISHA NA MUNGU"(Isaya 59:2). Halafu Omba "NGUVU YA MUNGU" Kukusaidia "USIRUDIE KUTENDA DHAMBI ILEILE"... Yesu Alisema, "MAANA PASIPO MIMI, NINYI HAMUWEZI NENO/ JAMBO LOLOTE" (Yohana 15:5). Kuishinda Dhambi, Si Kwa Akili Na Jitihada Ya Kimwili, "SI KWA NGUVU WALA SI KWA UWEZO BALI NI KWA ROHO WA BWANA" (Zekaria 4:6).
  3. Amua Kwa Dhati KUACHANA NA WATU "WANAOKUSHAWISHI" Au WANAOKUPELEKEA DHAMBINI"... "HERI MTU YULE ASIYEKWENDA KATIKA SHAURI LA WASIO HAKI [Watu Wasioipenda Haki Ya Mungu Na Neno Lake]... WALA HAKUSIMAMA KATIKA NJIA YA WAKOSAJI [Watu Ambao Wao Kutenda Makosa Ni Life Style Yao Na Hawajali Lolote]... WALA HAKUKETI BARAZANI PA WENYE MIZAHA [Makusanyiko Ya Watu Au Vijiwe Ambako Mambo Yasiyomtukuza Mungu Yanapewa Nafasi]"(Zaburi 1:1-2).
  4. Badili Mfumo Wako Wa Maisha, Toka Katika Ile Njia Ikupelekayo Dhambini Upesi... Amua Kuishi Kwa Ajili Ya Kumpendeza Mungu Kuliko Yeyote Au Chochote... HII INAHITAJI KUBADILI MFUMO WAKO WA MAWAZO [CHANGE OF MIND]... "MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII, BALI MFANYWE UPYA KWA KUGEUZWA NIA ZENU, MPATE KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU YALIYO MEMA, YA KUPENDEZA NA MAKAMILIFU" (Warumi 12:2).
  5. Dumu Kwenye Maombi Na Ushirika Na Mungu... MAOMBI YATAKUINGIZA KWENYE UWEPO WA MUNGU, NENO LAKE LITAKUFANYA USHIRIKIANE NAYE..."TENA IPOKEENI CHAPEO YA WOKOVU, NA UPANGA WA ROHO AMBAO NI NENO LA MUNGU. KWA SALA ZOTE NA MAOMBI MKISALI KILA WAKATI KATIKA ROHO, MKIKESHA KWA JAMBO HILO NA KUDUMU KATIKA KUWAOMBEA WATAKATIFU WOTE"(Waefeso 6:17-18).

Rumi 8:37 “Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.”

Search
Categories
Read More
Injili Ya Yesu Kristo
NAFASI YA MAWAZO KATIKA KUVIPIGA VITA VYA KIROHO
Vita vya kiroho, ni vita ambayo inapigwa katika ulimwengu wa roho, kwa jinsi ya rohoni baina ya...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:28:21 2 6K
Injili Ya Yesu Kristo
MAISHA BAADA YA KUBATIZWA NA ROHO MTAKATIFU.
Mtu anapozaliwa mara ya pili kwa kumkaribisha Bwana Yesu ndani ya maisha yake, huingia katika...
By GOSPEL PREACHER 2023-04-13 13:06:36 0 8K
OTHERS
MUHAMMAD ALIKUWA NA WAKE ZAIDI YA 20
Huu ni MSIBA mkubwa sana. Ifuatayo ni orodha ya wake wa Muhammad iliyoandaliwa na mwanazuoni wa...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:48:32 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
JINSI YA KUWASHINDA MAPEPO
Mstari wa Msingi  Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana (Struggle NIV,...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 00:58:05 0 10K
SPIRITUAL EDUCATION
Can Christians be demon-possessed?
No, Christians cannot be demon-possessed.  Possession implies ownership, and Christians are...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:58:01 0 5K