JINSI YA KUISHINDA DHAMBI JUMLA

0
5Кб
  1. Kubali Kwamba Umeitenda Hiyo Dhambi, Na Usijaribu Kutafuta ANDIKO LA KUJIHAMI, Au MTU WA KUMSINGIZIA..."AFICHAYE DHAMBI ZAKE HATAFANIKIWA, BALI AZIUNGAMAYE NA KUZIACHA, ATAPATA REHEMA"(Mithali 28:13).
  2. Ungama Dhambi Hiyo Kwa Lengo La Kutengeneza Na Mungu..."DHAMBI ZENU ZIMEWAFARAKANISHA NA MUNGU"(Isaya 59:2). Halafu Omba "NGUVU YA MUNGU" Kukusaidia "USIRUDIE KUTENDA DHAMBI ILEILE"... Yesu Alisema, "MAANA PASIPO MIMI, NINYI HAMUWEZI NENO/ JAMBO LOLOTE" (Yohana 15:5). Kuishinda Dhambi, Si Kwa Akili Na Jitihada Ya Kimwili, "SI KWA NGUVU WALA SI KWA UWEZO BALI NI KWA ROHO WA BWANA" (Zekaria 4:6).
  3. Amua Kwa Dhati KUACHANA NA WATU "WANAOKUSHAWISHI" Au WANAOKUPELEKEA DHAMBINI"... "HERI MTU YULE ASIYEKWENDA KATIKA SHAURI LA WASIO HAKI [Watu Wasioipenda Haki Ya Mungu Na Neno Lake]... WALA HAKUSIMAMA KATIKA NJIA YA WAKOSAJI [Watu Ambao Wao Kutenda Makosa Ni Life Style Yao Na Hawajali Lolote]... WALA HAKUKETI BARAZANI PA WENYE MIZAHA [Makusanyiko Ya Watu Au Vijiwe Ambako Mambo Yasiyomtukuza Mungu Yanapewa Nafasi]"(Zaburi 1:1-2).
  4. Badili Mfumo Wako Wa Maisha, Toka Katika Ile Njia Ikupelekayo Dhambini Upesi... Amua Kuishi Kwa Ajili Ya Kumpendeza Mungu Kuliko Yeyote Au Chochote... HII INAHITAJI KUBADILI MFUMO WAKO WA MAWAZO [CHANGE OF MIND]... "MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII, BALI MFANYWE UPYA KWA KUGEUZWA NIA ZENU, MPATE KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU YALIYO MEMA, YA KUPENDEZA NA MAKAMILIFU" (Warumi 12:2).
  5. Dumu Kwenye Maombi Na Ushirika Na Mungu... MAOMBI YATAKUINGIZA KWENYE UWEPO WA MUNGU, NENO LAKE LITAKUFANYA USHIRIKIANE NAYE..."TENA IPOKEENI CHAPEO YA WOKOVU, NA UPANGA WA ROHO AMBAO NI NENO LA MUNGU. KWA SALA ZOTE NA MAOMBI MKISALI KILA WAKATI KATIKA ROHO, MKIKESHA KWA JAMBO HILO NA KUDUMU KATIKA KUWAOMBEA WATAKATIFU WOTE"(Waefeso 6:17-18).

Rumi 8:37 “Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.”

Поиск
Категории
Больше
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 6
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 91 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-24 09:11:08 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
UKWELI KUHUSU HAKI IPATIKANAYO KWA IMANI
Leo ndugu zangu napenda kuzungumza haswa juu ya kuhesabiwa haki. Je, tunahesabiwaje? Je, kwa...
От PROSPER HABONA 2022-01-17 01:06:38 0 5Кб
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 18
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 32 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-22 17:56:24 0 5Кб
Religion
FUND FUND
Jeremiah Chapter 48 Verses 1-47: The Moabites were descendants of Lot who lived east of the...
От GOSPEL PREACHER 2021-12-31 20:47:38 0 6Кб
Injili Ya Yesu Kristo
AINA TATU ZA WAKRISTO
Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno matukufu ya uzima,...
От PROSPER HABONA 2022-01-23 04:38:19 0 8Кб