JINSI YA KUISHINDA DHAMBI JUMLA

0
5K
  1. Kubali Kwamba Umeitenda Hiyo Dhambi, Na Usijaribu Kutafuta ANDIKO LA KUJIHAMI, Au MTU WA KUMSINGIZIA..."AFICHAYE DHAMBI ZAKE HATAFANIKIWA, BALI AZIUNGAMAYE NA KUZIACHA, ATAPATA REHEMA"(Mithali 28:13).
  2. Ungama Dhambi Hiyo Kwa Lengo La Kutengeneza Na Mungu..."DHAMBI ZENU ZIMEWAFARAKANISHA NA MUNGU"(Isaya 59:2). Halafu Omba "NGUVU YA MUNGU" Kukusaidia "USIRUDIE KUTENDA DHAMBI ILEILE"... Yesu Alisema, "MAANA PASIPO MIMI, NINYI HAMUWEZI NENO/ JAMBO LOLOTE" (Yohana 15:5). Kuishinda Dhambi, Si Kwa Akili Na Jitihada Ya Kimwili, "SI KWA NGUVU WALA SI KWA UWEZO BALI NI KWA ROHO WA BWANA" (Zekaria 4:6).
  3. Amua Kwa Dhati KUACHANA NA WATU "WANAOKUSHAWISHI" Au WANAOKUPELEKEA DHAMBINI"... "HERI MTU YULE ASIYEKWENDA KATIKA SHAURI LA WASIO HAKI [Watu Wasioipenda Haki Ya Mungu Na Neno Lake]... WALA HAKUSIMAMA KATIKA NJIA YA WAKOSAJI [Watu Ambao Wao Kutenda Makosa Ni Life Style Yao Na Hawajali Lolote]... WALA HAKUKETI BARAZANI PA WENYE MIZAHA [Makusanyiko Ya Watu Au Vijiwe Ambako Mambo Yasiyomtukuza Mungu Yanapewa Nafasi]"(Zaburi 1:1-2).
  4. Badili Mfumo Wako Wa Maisha, Toka Katika Ile Njia Ikupelekayo Dhambini Upesi... Amua Kuishi Kwa Ajili Ya Kumpendeza Mungu Kuliko Yeyote Au Chochote... HII INAHITAJI KUBADILI MFUMO WAKO WA MAWAZO [CHANGE OF MIND]... "MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII, BALI MFANYWE UPYA KWA KUGEUZWA NIA ZENU, MPATE KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU YALIYO MEMA, YA KUPENDEZA NA MAKAMILIFU" (Warumi 12:2).
  5. Dumu Kwenye Maombi Na Ushirika Na Mungu... MAOMBI YATAKUINGIZA KWENYE UWEPO WA MUNGU, NENO LAKE LITAKUFANYA USHIRIKIANE NAYE..."TENA IPOKEENI CHAPEO YA WOKOVU, NA UPANGA WA ROHO AMBAO NI NENO LA MUNGU. KWA SALA ZOTE NA MAOMBI MKISALI KILA WAKATI KATIKA ROHO, MKIKESHA KWA JAMBO HILO NA KUDUMU KATIKA KUWAOMBEA WATAKATIFU WOTE"(Waefeso 6:17-18).

Rumi 8:37 “Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.”

Căutare
Categorii
Citeste mai mult
Injili Ya Yesu Kristo
MKRISTO NA UCHUMI: CHRISTOPHER MWAKASEGE
Utangulizi SI MAPENZI YA MUNGU TUWE MASIKINI! (Namna ya mkristo kuishi katika hali ngumu ya...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-19 07:19:55 0 12K
Injili Ya Yesu Kristo
YESU ANASEMA: MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA!
Leo nitajibu haya madai ya Upanga. Waumini wa dini ya Kiislam katika Mihadhara mbalimbali ya...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:16:31 0 5K
HOLY BIBLE
What did Jesus come to do?
To reveal the Father (Matt. 11:27) "All things have been committed to me by my Father. No...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:54:43 0 5K
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:53:56 0 5K
NDOA KIBIBLIA
MWANAUME: SIO MKE WAKO NI WEWE
Mchungaji wangu Emmanuel Nhyama Manwele ambaye ni mwalimu wangu wa kwanza wa ndoa na maswala...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:15:02 0 6K