YESU NDIE NJIA NA KWELI NA UZIMA. Kumbe Dini sio Njia

0
5KB
Katika Biblia tunasoma kuwa Yesu anasema yeye ndie "KWELI" na anaendelea kusema kuwa KWELI ndiyo itakuweka HURU. Hebu rejea kwenye hii aya: 

Yohana 14:6 Yesu akawaambia, “Mimi ndiye Njia na Kweli na Uzima; mtu hawezi kufika kwa Baba bila kupitia kwangu.

Kufuatana na aya hapo juu, Mtu yeyote yule hawezi kwenda kwa Baba na/au Mbiguni bila ya kupitia "KWELI" ambayo ni YESU. Kumbe basi dini haiwezi kukupeleka popote pale. Kumbe, NJIA PEKEE ya Uzima wa Milele ni YESU na SI DINI.

Kumfahamu Yesu ambaye ni KWELI kutakufanya umwelewe Mungu wa UKWELI!! Kumbe basi, Yesu ndie mwenye uwezo wa kukufanya uelewe KWELI ya Mungu.

Yohana 8:31-32 Kwa hiyo Yesu akawaambia wale waliomwamini, “Kama mkiendelea kutii maneno yangu mtakuwa wanafunzi wangu halisi. 32 Mtaelewa yaliyo kweli kumhusu Mungu na ukweli huu utawafanya muwe watu huru.

Kufuatana na aya hapo juu, inatuhakikishia kuwa mafundisho ya YESU PEKEE ndiyo yatakufanya uelewe KWELI na kumfahamu Mungu wa KWELI. Zaidi ya hapo, kuwa Mwanafunzi wa Yesu(Ukristo) ndio njia pekee ya kufahamu kweli.

Yesu Ndie Njia ya Kweli na Uzima.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 62 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:02:27 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
PASIPO UTAKATIFU NA AMANI HAIZEKANI KUMUONA MUNGU (EBRANIA 12:14 PART 01:)
PASIPO UTAKATIFU NA AMANI HAIZEKANI KUMUONA MUNGU (EBRANIA 12:14 PART 01:)
Par Martin Laizer 2023-10-18 11:55:36 2 8KB
SPIRITUAL EDUCATION
Spirit, Soul, and Body
The Christian doctrine of immortality cannot be understood apart from the right conception of...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:38:37 0 5KB
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
GFG
FDF
Par GOSPEL PREACHER 2021-12-31 12:37:18 0 5KB
REVELATION
UFUNUO 15
Karibu tujifunze mwendelezo wa kitabu cha ufunuo, leo tukiendelea na sura ya 15; Ufunuo...
Par GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:50:48 0 6KB