NINI MAANA YA MTU KUZIKWA NDANI YA KANISA? KATIKA NYUMBA YA IBADA?

0
5KB

Ukisoma katika kitabu cha Mathayo 22:32 inasema mimi ni MUNGU wa Ibrahim, na MUNGU Isaka, na MUNGU wa Yakobo. MUNGU si MUNGU wa wafu, bali wa walio hai. Sisi sote ni kizazi cha Ibrahimu ambaye MUNGU wake ndiye aliyekuwa MUNGU wa walio hai yaani watu wenye uhai na siyo waliokufa. Sasa ninachofundisha hapa ni watu kuelewa ukweli wasipotee wakifikiri wanamwabudu MUNGU aliye hai bali inakuwa ni upofu wa macho pasipo watu kujua au kuelewa waliabudu mahali ambapo upo mzoga au mauti ndani ya kanisa. Inapokuwa mtu amezikwa ndani ya kanisa au kupeleka maiti yake au mifupa basi tayari madhabahu hiyo inakuwa ni ya mungu wa wafu ndiye atawalaye na watu wataongozwa na mungu mfu.

Ukisoma katika biblia baba yetu Ibrahimu mwenyewe aliyembarikiwa yeye hajazikwagwa ndani ya kanisa au hekalu, pia YESU mwenyewe mwana wa MUNGU maiti yake haikuzikwa kanisani alizikwa mbali sababu madhabahuni ni mahali patakatifu pa MUNGU aliye hai na yeye ndiye hukaa pale, na inapofanyika maiti inazikwa pale inabadilika mara moja anakuja kuishi mungu wa wafu, na ukisoma biblia utaona MUNGU amekataa yeye ni MUNGU aliye hai maiti izikwe pale iozee pale? Na zaidi ukisoma katika kitabu cha Marko 12: 27, neno linasema yeye si MUNGU wa wafu bali ni MUNGU wa walio hai. Hivyo  wapotea sana, maeneo haya aliyasema MUNGU ya kuwa mwapotea sana yaani kupita kiasi na bila kujua katika ulimwengu huu. Ndiye sababu hataki  ibada za wafu ila leo zipo na kama zipo zinafanywa basi waelewe wafanyao hayo wao wapo chini ya mungu mfu. Sasa ni wakati wa kumrejea MUNGU wa kweli na siyo mungu wa wafu. Na wewe unayependa kuwa chini ya MUNGU wa uhai inakupasa kujitenge na mambo ya wafu na hata kuzikiwa vitu au makaburi kujengwa kanisani au katika madhabahu, inapokuwa ni hivyo basi hapo shetani anapata nafasi ya kuwateka watu wale sababu tu ya wafu

Kila mtu anajua ukisoma Marko 11: 15-18 hata YESU alipoingia katika hekalu alikuta waliofanya mambo ya biashara, alijua tayari MUNGU siyo mahali pake tena hivyo ili pawe na MUNGU aliye hai aliviondoa na kuwafukuza hekalu likabaki safi na MUNGU akatukuzwa. Na zaidi hata kibinadamu mtu ukikaa karibu na kaburi unaogopa linatisha, sababu katika kaburi inaishi roho ya mauti na ikiwa ni hivyo basi uelewe na madhabahu hizo zinaishi roho za mauti na mahali palipo na mauti anaishi mungu wa wafu. Hivyo unapoona hivyo uelewe ni mahali pa mungu wa wafu asiye na uhai na wanaoabudu hapo watashikiliwa na mungu mfu sababu anacho kibali, mahali unaposali ndipo na baraka za maisha yako yaliopo. Ikiwa kuna uzima utapata uzima, ikiwa kuna wafu utapata umaiti na kuhukumiwa usiende mbinguni.

Suche
Kategorien
Mehr lesen
Injili Ya Yesu Kristo
HAKIMU ALIYE TOFAUTI NA MAHAKIMU WOTE
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary...
Von GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:34:25 0 5KB
OTHERS
Waislam Wauliza Wakristo
  Swali la 1: Kwa nini mnaliamini Agano la Kale? Jibu: Maandiko na elimukale...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:40:11 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
NAMNA YA KUJENGA MAHUSIANO MAZURI NA ROHO MTAKATIFU.
Yohana 14:16-17. Biblia inasema “ Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:59:31 0 5KB
OTHERS
The 20 Versions of the Qur'an today. (7 are recorded in the Hadith.)
The Muslim Claim that the Qur'an is unchanged:No other book in the world can match the...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:43:46 0 5KB
MASWALI & MAJIBU
Bwana Aliposema Kuwa Yeye Ni “Mungu Wa Miungu” Alikuwa Na Maana Gani?..Je! Yeye Ni Mungu Wa Sanamu?
JIBU: Tukisoma Kumbukumbu 10:17 inasema… “Kwa maana Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye...
Von GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:14:03 0 6KB