NINI MAANA YA MTU KUZIKWA NDANI YA KANISA? KATIKA NYUMBA YA IBADA?

0
5KB

Ukisoma katika kitabu cha Mathayo 22:32 inasema mimi ni MUNGU wa Ibrahim, na MUNGU Isaka, na MUNGU wa Yakobo. MUNGU si MUNGU wa wafu, bali wa walio hai. Sisi sote ni kizazi cha Ibrahimu ambaye MUNGU wake ndiye aliyekuwa MUNGU wa walio hai yaani watu wenye uhai na siyo waliokufa. Sasa ninachofundisha hapa ni watu kuelewa ukweli wasipotee wakifikiri wanamwabudu MUNGU aliye hai bali inakuwa ni upofu wa macho pasipo watu kujua au kuelewa waliabudu mahali ambapo upo mzoga au mauti ndani ya kanisa. Inapokuwa mtu amezikwa ndani ya kanisa au kupeleka maiti yake au mifupa basi tayari madhabahu hiyo inakuwa ni ya mungu wa wafu ndiye atawalaye na watu wataongozwa na mungu mfu.

Ukisoma katika biblia baba yetu Ibrahimu mwenyewe aliyembarikiwa yeye hajazikwagwa ndani ya kanisa au hekalu, pia YESU mwenyewe mwana wa MUNGU maiti yake haikuzikwa kanisani alizikwa mbali sababu madhabahuni ni mahali patakatifu pa MUNGU aliye hai na yeye ndiye hukaa pale, na inapofanyika maiti inazikwa pale inabadilika mara moja anakuja kuishi mungu wa wafu, na ukisoma biblia utaona MUNGU amekataa yeye ni MUNGU aliye hai maiti izikwe pale iozee pale? Na zaidi ukisoma katika kitabu cha Marko 12: 27, neno linasema yeye si MUNGU wa wafu bali ni MUNGU wa walio hai. Hivyo  wapotea sana, maeneo haya aliyasema MUNGU ya kuwa mwapotea sana yaani kupita kiasi na bila kujua katika ulimwengu huu. Ndiye sababu hataki  ibada za wafu ila leo zipo na kama zipo zinafanywa basi waelewe wafanyao hayo wao wapo chini ya mungu mfu. Sasa ni wakati wa kumrejea MUNGU wa kweli na siyo mungu wa wafu. Na wewe unayependa kuwa chini ya MUNGU wa uhai inakupasa kujitenge na mambo ya wafu na hata kuzikiwa vitu au makaburi kujengwa kanisani au katika madhabahu, inapokuwa ni hivyo basi hapo shetani anapata nafasi ya kuwateka watu wale sababu tu ya wafu

Kila mtu anajua ukisoma Marko 11: 15-18 hata YESU alipoingia katika hekalu alikuta waliofanya mambo ya biashara, alijua tayari MUNGU siyo mahali pake tena hivyo ili pawe na MUNGU aliye hai aliviondoa na kuwafukuza hekalu likabaki safi na MUNGU akatukuzwa. Na zaidi hata kibinadamu mtu ukikaa karibu na kaburi unaogopa linatisha, sababu katika kaburi inaishi roho ya mauti na ikiwa ni hivyo basi uelewe na madhabahu hizo zinaishi roho za mauti na mahali palipo na mauti anaishi mungu wa wafu. Hivyo unapoona hivyo uelewe ni mahali pa mungu wa wafu asiye na uhai na wanaoabudu hapo watashikiliwa na mungu mfu sababu anacho kibali, mahali unaposali ndipo na baraka za maisha yako yaliopo. Ikiwa kuna uzima utapata uzima, ikiwa kuna wafu utapata umaiti na kuhukumiwa usiende mbinguni.

Pesquisar
Categorias
Leia mais
UCHUMBA KIBIBLIA
UCHUMBA NI NINI? NA NDOA NI NINI?
Shalom, wapendwa,Katika somo letu leo nataka tuangalie vitu hivi viwili, mahusiano ya uchumba na...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-06 13:06:36 0 7KB
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-02-05 13:41:13 0 6KB
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-03-20 05:06:10 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
HEKIMA YA KUJIBU MASWALI
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
Por GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:44:46 0 5KB
NEHEMIAH
Verse by verse explanation of Nehemiah 6
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-04-02 12:22:32 0 6KB