NINI MAANA YA MTU KUZIKWA NDANI YA KANISA? KATIKA NYUMBA YA IBADA?

0
5K

Ukisoma katika kitabu cha Mathayo 22:32 inasema mimi ni MUNGU wa Ibrahim, na MUNGU Isaka, na MUNGU wa Yakobo. MUNGU si MUNGU wa wafu, bali wa walio hai. Sisi sote ni kizazi cha Ibrahimu ambaye MUNGU wake ndiye aliyekuwa MUNGU wa walio hai yaani watu wenye uhai na siyo waliokufa. Sasa ninachofundisha hapa ni watu kuelewa ukweli wasipotee wakifikiri wanamwabudu MUNGU aliye hai bali inakuwa ni upofu wa macho pasipo watu kujua au kuelewa waliabudu mahali ambapo upo mzoga au mauti ndani ya kanisa. Inapokuwa mtu amezikwa ndani ya kanisa au kupeleka maiti yake au mifupa basi tayari madhabahu hiyo inakuwa ni ya mungu wa wafu ndiye atawalaye na watu wataongozwa na mungu mfu.

Ukisoma katika biblia baba yetu Ibrahimu mwenyewe aliyembarikiwa yeye hajazikwagwa ndani ya kanisa au hekalu, pia YESU mwenyewe mwana wa MUNGU maiti yake haikuzikwa kanisani alizikwa mbali sababu madhabahuni ni mahali patakatifu pa MUNGU aliye hai na yeye ndiye hukaa pale, na inapofanyika maiti inazikwa pale inabadilika mara moja anakuja kuishi mungu wa wafu, na ukisoma biblia utaona MUNGU amekataa yeye ni MUNGU aliye hai maiti izikwe pale iozee pale? Na zaidi ukisoma katika kitabu cha Marko 12: 27, neno linasema yeye si MUNGU wa wafu bali ni MUNGU wa walio hai. Hivyo  wapotea sana, maeneo haya aliyasema MUNGU ya kuwa mwapotea sana yaani kupita kiasi na bila kujua katika ulimwengu huu. Ndiye sababu hataki  ibada za wafu ila leo zipo na kama zipo zinafanywa basi waelewe wafanyao hayo wao wapo chini ya mungu mfu. Sasa ni wakati wa kumrejea MUNGU wa kweli na siyo mungu wa wafu. Na wewe unayependa kuwa chini ya MUNGU wa uhai inakupasa kujitenge na mambo ya wafu na hata kuzikiwa vitu au makaburi kujengwa kanisani au katika madhabahu, inapokuwa ni hivyo basi hapo shetani anapata nafasi ya kuwateka watu wale sababu tu ya wafu

Kila mtu anajua ukisoma Marko 11: 15-18 hata YESU alipoingia katika hekalu alikuta waliofanya mambo ya biashara, alijua tayari MUNGU siyo mahali pake tena hivyo ili pawe na MUNGU aliye hai aliviondoa na kuwafukuza hekalu likabaki safi na MUNGU akatukuzwa. Na zaidi hata kibinadamu mtu ukikaa karibu na kaburi unaogopa linatisha, sababu katika kaburi inaishi roho ya mauti na ikiwa ni hivyo basi uelewe na madhabahu hizo zinaishi roho za mauti na mahali palipo na mauti anaishi mungu wa wafu. Hivyo unapoona hivyo uelewe ni mahali pa mungu wa wafu asiye na uhai na wanaoabudu hapo watashikiliwa na mungu mfu sababu anacho kibali, mahali unaposali ndipo na baraka za maisha yako yaliopo. Ikiwa kuna uzima utapata uzima, ikiwa kuna wafu utapata umaiti na kuhukumiwa usiende mbinguni.

Buscar
Categorías
Read More
OTHERS
ALLAH NI MUONGO KUTOKANA NA BIBLIA NA KORAN
Je, Allah ndiye Shetani yule yule ? Katika ujumbe wa leo, nitaweka ushaidi wa Kibiblia na Koran...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:12:00 0 6K
OTHERS
WAKRISTO JIEPUSHENI NA SALAAM MNAYOSALIMIWA NA WAISLAMU
Imekuwa ni desturi kuwasikia, au kumsikia Muislamu, akimsalimia Mkristo, Sam aleykum (سم عليكم)...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:54:09 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
THE TRUTH ABOUT RIGHTEOUSNESS FOUND IN FAITH
Today, brethren, I would like to talk specifically about justification. How are we counted? By...
By PROSPER HABONA 2022-01-17 01:18:01 0 6K
MASWALI & MAJIBU
Mungu Alikuwa Anaongea Na Nani Aliposema Na “Tumfanye Mtu Kwa Mfano Wetu”,(Mwanzo 1:26)?
Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:18:49 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
KWA NINI IMANI YA MWANAMKE MKANANAYO ILIONEKANA KUWA KUBWA?
Nakusalimu kwa jina la Bwana, amani na iwe kwako. Katika Mathayo 15:21-28 maandiko...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:17:48 0 5K