Ukijibu Kabla Haujasikia, Ni Upumbavu Na Aibu Kwako.

0
6K

Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,  Ni upumbavu na aibu kwake.


Hekima inatufundisha tusiwe watu wa kujibu au kuzungumza kabla hatujasikia habari yote au taaarifa yote na kuitafakari kwanza..Kwamfano mwenzako anazungumza jambo Kisha wewe ukaingilia kati na kutaka kujibu, hoja ambayo haijakamilika..Matokeo yake hapo ni Nini kama sio kutoa majibu yasiyosahihi?. Au ambayo hayajakamilika?

Ndio hapo anasema ni upumbavu na aibu kwake. 

Hii imeathiri hata kusambaa Kwa taaarifa za uongo. Mtu atasikia jambo, kwasababu Hana taaarifa nalo vizuri, atatoka muda huo huo na kwenda kumpasha mwingine, na yule mwingine atampasha mwingine..Hivyo taaarifa za uongo huzagaa Kwa upesi sana. Ndivyo ambavyo hata waandishi wa habari ambao hawawi makini wanavyosambaza habari ambazo bado hawajazifanyia uchambuzi yakinifu. Na matokeo yake husababisha matatizo makubwa katika jamii. 

Mafarisayo na wayahudi walimpinga Yesu kwasababu walikuwa ni watu wa kupokea tu taaarifa ambazo hawazitafiti, walisikia Yesu anatokea Nazareti, wakahitimisha amezaliwa Nazareti, wengine wakamwita Msamaria. Lakini kama wangesubiri kutuatilia Kwa ukaribu mawazo Yao yangebadilika, na wasingekuwa wapumbavu kama tunavyowasoma kwenye biblia.

Hata wakati alipokuwa anazungumza nao, hawakutaka kusikiliza mpaka mwisho ni Nini Bwana anataka kuwaambia, kwamfano Kuna wakati aliwaambia, mtu akilishika Neno lake hataonja mauti milele. Lakini wao Hawakutaka ufafanuzi alimaanisha Nini.. hapo hapo wakarukia na kumwita ana Pepo;Kwa kauli Ile.

Yohana 8:52-53

[52]Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.

[53]Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?

Wakati mwingine aliwaambia livunjeni hili hekalu,nami nitalisimamisha baada ya siku tatu. Wakairukia hiyo kauli bila kusubiria maelezo  yake , ndio ikawa habari ya mji mzima Kuna mtu kasema anaweza kulijenga Kwa siku 3 hekalu lililojengwa Kwa miaka 46. Kumbe hawakujua Kristo anazungumzia habari ya mwili wake.(Yohana 2:20)

Biblia inatuasa tuwe wepesi wa kusikia, na si wa kusema; Ina faida nyingi.

Yakobo 1:19

[19]Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Bwana akubariki.

Like
1
Zoeken
Categorieën
Read More
SPIRITUAL EDUCATION
What does the Bible say about sex before marriage?
There is no Hebrew or Greek word used in the Bible that precisely refers to sex before marriage....
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:27:04 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
UHUSIANO WA JINA NA HATMA YA MTU 1SAMWEL 25:25, MWANZO 32:24-28
UHUSIANO WA JINA NA HATMA YA MTU. 1SAMWEL 25:25, MWANZO 32:24-28. Moja kati ya teso kubwa la...
By Martin Laizer 2025-11-05 04:53:38 2 746
HOLY BIBLE
Will more people go to heaven or to hell?
The question of whether there are more people in heaven or hell is answered by Jesus Himself in...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:21:07 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
ROHO MTAKATIFU
Ndugu msomaji; Je, unamfahamu Roho Mtakatifu? Je, Roho Mtakatifu ni nani kwako?   Katika...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:33:29 0 5K
Religion
MASWALI NA MAJIBU KUHUSU DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU
Kumekuwepo na mijadala mingi kila mahali na pia kumewepo na maoni mengi ya watu na mawao tofauti...
By GOSPEL PREACHER 2021-08-24 13:00:08 0 7K