Ukijibu Kabla Haujasikia, Ni Upumbavu Na Aibu Kwako.

0
6χλμ.

Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,  Ni upumbavu na aibu kwake.


Hekima inatufundisha tusiwe watu wa kujibu au kuzungumza kabla hatujasikia habari yote au taaarifa yote na kuitafakari kwanza..Kwamfano mwenzako anazungumza jambo Kisha wewe ukaingilia kati na kutaka kujibu, hoja ambayo haijakamilika..Matokeo yake hapo ni Nini kama sio kutoa majibu yasiyosahihi?. Au ambayo hayajakamilika?

Ndio hapo anasema ni upumbavu na aibu kwake. 

Hii imeathiri hata kusambaa Kwa taaarifa za uongo. Mtu atasikia jambo, kwasababu Hana taaarifa nalo vizuri, atatoka muda huo huo na kwenda kumpasha mwingine, na yule mwingine atampasha mwingine..Hivyo taaarifa za uongo huzagaa Kwa upesi sana. Ndivyo ambavyo hata waandishi wa habari ambao hawawi makini wanavyosambaza habari ambazo bado hawajazifanyia uchambuzi yakinifu. Na matokeo yake husababisha matatizo makubwa katika jamii. 

Mafarisayo na wayahudi walimpinga Yesu kwasababu walikuwa ni watu wa kupokea tu taaarifa ambazo hawazitafiti, walisikia Yesu anatokea Nazareti, wakahitimisha amezaliwa Nazareti, wengine wakamwita Msamaria. Lakini kama wangesubiri kutuatilia Kwa ukaribu mawazo Yao yangebadilika, na wasingekuwa wapumbavu kama tunavyowasoma kwenye biblia.

Hata wakati alipokuwa anazungumza nao, hawakutaka kusikiliza mpaka mwisho ni Nini Bwana anataka kuwaambia, kwamfano Kuna wakati aliwaambia, mtu akilishika Neno lake hataonja mauti milele. Lakini wao Hawakutaka ufafanuzi alimaanisha Nini.. hapo hapo wakarukia na kumwita ana Pepo;Kwa kauli Ile.

Yohana 8:52-53

[52]Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.

[53]Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?

Wakati mwingine aliwaambia livunjeni hili hekalu,nami nitalisimamisha baada ya siku tatu. Wakairukia hiyo kauli bila kusubiria maelezo  yake , ndio ikawa habari ya mji mzima Kuna mtu kasema anaweza kulijenga Kwa siku 3 hekalu lililojengwa Kwa miaka 46. Kumbe hawakujua Kristo anazungumzia habari ya mwili wake.(Yohana 2:20)

Biblia inatuasa tuwe wepesi wa kusikia, na si wa kusema; Ina faida nyingi.

Yakobo 1:19

[19]Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Bwana akubariki.

Like
1
Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
HOLY BIBLE
If Jesus is God, then why did He say the Father was greater than He?
"You heard that I said to you, ‘I go away, and I will come to you.’  If you...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:04:05 0 6χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
HEKIMA YA KUJIBU MASWALI
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
από GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:44:46 0 5χλμ.
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-01 22:13:11 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
Nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwaajili ya Kristo!
Wafilipi 3:4-11 “Walakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu ye yote akijiona kuwa anayo...
από GOSPEL PREACHER 2022-03-31 14:59:34 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
UTHIBITISHO KUWA YESU NI MUNGU
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
από GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:47:09 0 6χλμ.