KUPENDANA HUSITIRI DHAMBI

0
6KB
Ndugu zangu,
Nawasalimu katika jina la Yesu. Mungu mwema kwa neema zake leo tena tumepata neema ya kumtumikia. 
Napenda tumtafakari Mungu kwa maneno haya machache. Mtume Petro anasema "Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi" - 1 Petro 4:8
 
Kuna msemo wa kiswahili wanasema 'kupenda ni upofu'! Wanasema unapompenda mtu hata zile kasoro ambazo wengine wanaziona kwa huyo umpendae basi wewe huzioni. Sababu ni moja tu, Upendo husitiri dhambi wana wa Mungu.  Na mtume Petro anatukumbusha tuwe na bidii katika kupendana. Ndugu zangu tukiwa na bidii katika kupendana ndani ya jamii zetu, ndani ya madhehebu yetu, ndani ya ofisi zetu, ndani ya maeneo yetu tunayofanyia kazi, ndani ya mashambani mwetu, nakuambia katika jina la Yesu hutaona tofauti unazoziona kwa jirani yako au ndugu yako kama unavyoziona sasa. Lakini kwa sababu tu hatujatia bidii katika kupendana ndo maana tunaona hivi vitofauti vidogo vidogo hadi vinaibukia kututenganisha na kutufarakanisha.
 
Mwandishi wa Mithali 10:12 anasema "Kuchukiana huondokesha fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote"!.  Ndani ya ndoa zetu kumbe tukipendana viji-ugomvi visivyo na kichwa wala miguu hatutaviona wapendwa wana wa Mungu kwa sababu kuchukiana ndiko kunakoleta fitina. Tena "Upendo huvumilia" - 1Kor 13:4 ndio maana unakuwa kipofu kwa udhaifu kwa mwenzio.
 
Ndugu yangu ni ombi langu siku ya leo Roho Mtakatifu akusaidie uwe na bidii katika kupendana. Kwa maana kupendana kunasitiri dhambi mtumishi wa Mungu nakuambia. Inawezekana ndugu yako au jamaa yako au rafiki yako amekukosea au amekuwa akikukosea mara kwa mara ndo maana hutaki tena kumpenda. Lakini laiti Mungu angehesabu makosa yetu nadhani dunia hii tungekuwa tunapukutika kila siku. Basi nakuombea Roho Mtakatifu arudishe upendo wako wa kwanza na sasa uendelee mbele katika kupendana na jirani yako, na ndugu yako na rafiki yako. Mwambie Roho wa Mungu akusidie kupendana. Kwa nguvu zetu hatuwezi. Hebu omba neema ya Mungu katika hili.
 
Mungu akubariki sana.
Like
1
Rechercher
Catégories
Lire la suite
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 22 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:16:50 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
NINI MAANA YA MTU KUZIKWA NDANI YA KANISA? KATIKA NYUMBA YA IBADA?
Ukisoma katika kitabu cha Mathayo 22:32 inasema mimi ni MUNGU wa Ibrahim, na MUNGU Isaka, na...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:43:45 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
HAZINA YA MTU
PALIPO NA HAZINA YA MTU NDIPO NA MOYO WAKE UTAKAPOKUWA 
Par Martin Laizer 2023-09-25 06:09:55 0 14KB
Injili Ya Yesu Kristo
DINI YA KIISLAM ILIANZISHWA SIKU YA JUMATATU MWEZI WA 17, SAWA SAWA NA TAREHE 27 DESEMBA MKWA 610 B.K.
KUMBE UISLAM NI DINI YA KUTENGEZA TU, TENA CHANGA SANA NA HAIKUWEPO KABLA YA MUHAMMAD  ...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:13:31 0 6KB
Religion
USHUHUDA WA MAONO YA JEHANAMU NA YERUSALEMU MPYA WA NYISAKI CHAULA
  UTANGULIZI: Sura ya 1: Kuitwa Sura ya 2: Jehanamu sehemu ya kwanza na Mangojeo ya Wafu....
Par GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:21:26 0 6KB