KUPENDANA HUSITIRI DHAMBI

0
6KB
Ndugu zangu,
Nawasalimu katika jina la Yesu. Mungu mwema kwa neema zake leo tena tumepata neema ya kumtumikia. 
Napenda tumtafakari Mungu kwa maneno haya machache. Mtume Petro anasema "Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi" - 1 Petro 4:8
 
Kuna msemo wa kiswahili wanasema 'kupenda ni upofu'! Wanasema unapompenda mtu hata zile kasoro ambazo wengine wanaziona kwa huyo umpendae basi wewe huzioni. Sababu ni moja tu, Upendo husitiri dhambi wana wa Mungu.  Na mtume Petro anatukumbusha tuwe na bidii katika kupendana. Ndugu zangu tukiwa na bidii katika kupendana ndani ya jamii zetu, ndani ya madhehebu yetu, ndani ya ofisi zetu, ndani ya maeneo yetu tunayofanyia kazi, ndani ya mashambani mwetu, nakuambia katika jina la Yesu hutaona tofauti unazoziona kwa jirani yako au ndugu yako kama unavyoziona sasa. Lakini kwa sababu tu hatujatia bidii katika kupendana ndo maana tunaona hivi vitofauti vidogo vidogo hadi vinaibukia kututenganisha na kutufarakanisha.
 
Mwandishi wa Mithali 10:12 anasema "Kuchukiana huondokesha fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote"!.  Ndani ya ndoa zetu kumbe tukipendana viji-ugomvi visivyo na kichwa wala miguu hatutaviona wapendwa wana wa Mungu kwa sababu kuchukiana ndiko kunakoleta fitina. Tena "Upendo huvumilia" - 1Kor 13:4 ndio maana unakuwa kipofu kwa udhaifu kwa mwenzio.
 
Ndugu yangu ni ombi langu siku ya leo Roho Mtakatifu akusaidie uwe na bidii katika kupendana. Kwa maana kupendana kunasitiri dhambi mtumishi wa Mungu nakuambia. Inawezekana ndugu yako au jamaa yako au rafiki yako amekukosea au amekuwa akikukosea mara kwa mara ndo maana hutaki tena kumpenda. Lakini laiti Mungu angehesabu makosa yetu nadhani dunia hii tungekuwa tunapukutika kila siku. Basi nakuombea Roho Mtakatifu arudishe upendo wako wa kwanza na sasa uendelee mbele katika kupendana na jirani yako, na ndugu yako na rafiki yako. Mwambie Roho wa Mungu akusidie kupendana. Kwa nguvu zetu hatuwezi. Hebu omba neema ya Mungu katika hili.
 
Mungu akubariki sana.
Like
1
Rechercher
Catégories
Lire la suite
NEHEMIAH
Verse by verse explanation of Nehemiah 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 27 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-02 12:34:25 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
Kweli 100 Kuhusu Yesu
1. Yesu alidai kuwa Mungu, (Yohana 8:24, 8: 56-59 (angalia Kutoka 3:14), Yohana 10: 30-33) 2....
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 06:20:18 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
VIFUNGO.
Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi; Neno “vifungo“ni neno la wingi kutoka neno...
Par GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:18:35 0 5KB
HOLY BIBLE
If Jesus is God, then why did He say the Father was greater than He?
"You heard that I said to you, ‘I go away, and I will come to you.’  If you...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:04:05 0 5KB
Religion
HOW TO BECOME A CHRISTIAN?
This question is very important, and not all human beings know its answer. But it is very simple...
Par GOSPEL PREACHER 2021-08-25 10:01:32 0 5KB