Ni Sahihi Kumuita Mariamu Mama Wa Mungu?

0
7χλμ.

Kwa kuwa Bwana Yesu alipitia katika tumbo la Mariamu je! Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

JIBU: Mariamu alimzaa BWANA kwa namna ya mwili, hivyo wakati Bwana alipokuwa duniani ndio Mariamu alijulikana kama mama wa Yesu, na sio mama wa Mungu. Bwana Yesu alipokuja hapa duniani alikuwa ni Mungu katika mwili lakini hakuja kutafuta kuabudiwa na ndio maana hakuna sehemu yoyote alijiita yeye ni Mungu, zaidi sana alikuwa anawarudisha watu wamuabudu Baba.   Kumbuka Mungu alipouvaa mwili ilimpasa afananishwe na mwanadamu kwa namna zote, azaliwe, ale chakula, asikie maumivu, alie, aone huruma, n.k. kama mwanadamu mwingine yeyote, si ajabu kumuona akiwa na Baba au bibi, au babu au mjomba, lakini haimaanishi kuwa yeye (YESU) yupo chini ya hao wote hapana..

Biblia inatueleza vizuri juu ya jambo hilo tukisoma katika..

Mathayo 22:41 Bwana Yesu alizungumza maneno haya;  

“41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo? 42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi. 43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema, 44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako? 45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe? 46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena”.

Unaona hapo? jibu litakuwa pia hivyo hivyo kwa Mariamu kwamba Yesu atakuwaje mwanawe na wakati bado ni Bwana wake? na yeye ni binti wa Mungu (Kwasababu kama Daudi alikuwa mkubwa kuliko Mariamu aliambiwa hivyo je! si zaidi yeye?).  

Hivyo sisi wote tunaomwamini YESU KRISTO mbele zake ni ndugu na dada, Na yeye akiwa kama Baba yetu. Kwahiyo ni muhimu tujue kutofautisha jinsi Mungu anavyotenda kazi katika ofisi zake tofauti, Mungu anapoonyesha unyenyekevu (kuzaliwa kibinadamu) haimaanishi kuwa mwanadamu yupo juu yake. Hapana anafanya hivyo kutuonyesha sisi njia bora kama watoto wake.  

Ubarikiwe sana.


Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
Injili Ya Yesu Kristo
JE, UNAJUA KUZIMU NI WAPI?
JE UNAJUA KUZIMU IPO KATIKA ARDHI YA NCHI ZIPI KATIKA RAMANI YA DUNIA? BWANA YESU ASIFIWE, YESU...
από GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:55:07 0 5χλμ.
DARASA LA 6
DARASA LA 6
Orodha ya masomo yote ya darasa la 6
από PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:17:05 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
Mpango Wa Wokovu ni nini?
Una njaa? Si njaa ya chakula, lakini je, una njaa ya kitu Fulani zaidi maishani? Je, kuna hali...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:10:21 0 5χλμ.
SPIRITUAL EDUCATION
Tuliangalie fundisho la uongo kuwa ‘ukiokoka, umeokolewa milele (the false doctrine of Once saved always saved, OSAS)
Fundisho la uongo kuwa “mtu akisha okoka, ameokoka siku zote” linafundisha kwamba...
από PROSPER HABONA 2022-01-16 14:48:21 0 6χλμ.
OTHERS
Yesu Kristo hajaumbwa bali alikuwepo tangu milele yote
Ni kweli kabisa kwamba Yesu alikuwepo tangu milele yote kabla ya kuumbwa kitu cho chote kile....
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:58:23 0 5χλμ.