Ni Sahihi Kumuita Mariamu Mama Wa Mungu?

0
7Кб

Kwa kuwa Bwana Yesu alipitia katika tumbo la Mariamu je! Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

JIBU: Mariamu alimzaa BWANA kwa namna ya mwili, hivyo wakati Bwana alipokuwa duniani ndio Mariamu alijulikana kama mama wa Yesu, na sio mama wa Mungu. Bwana Yesu alipokuja hapa duniani alikuwa ni Mungu katika mwili lakini hakuja kutafuta kuabudiwa na ndio maana hakuna sehemu yoyote alijiita yeye ni Mungu, zaidi sana alikuwa anawarudisha watu wamuabudu Baba.   Kumbuka Mungu alipouvaa mwili ilimpasa afananishwe na mwanadamu kwa namna zote, azaliwe, ale chakula, asikie maumivu, alie, aone huruma, n.k. kama mwanadamu mwingine yeyote, si ajabu kumuona akiwa na Baba au bibi, au babu au mjomba, lakini haimaanishi kuwa yeye (YESU) yupo chini ya hao wote hapana..

Biblia inatueleza vizuri juu ya jambo hilo tukisoma katika..

Mathayo 22:41 Bwana Yesu alizungumza maneno haya;  

“41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo? 42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi. 43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema, 44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako? 45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe? 46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena”.

Unaona hapo? jibu litakuwa pia hivyo hivyo kwa Mariamu kwamba Yesu atakuwaje mwanawe na wakati bado ni Bwana wake? na yeye ni binti wa Mungu (Kwasababu kama Daudi alikuwa mkubwa kuliko Mariamu aliambiwa hivyo je! si zaidi yeye?).  

Hivyo sisi wote tunaomwamini YESU KRISTO mbele zake ni ndugu na dada, Na yeye akiwa kama Baba yetu. Kwahiyo ni muhimu tujue kutofautisha jinsi Mungu anavyotenda kazi katika ofisi zake tofauti, Mungu anapoonyesha unyenyekevu (kuzaliwa kibinadamu) haimaanishi kuwa mwanadamu yupo juu yake. Hapana anafanya hivyo kutuonyesha sisi njia bora kama watoto wake.  

Ubarikiwe sana.


Поиск
Категории
Больше
SPIRITUAL EDUCATION
PASIPO UTAKATIFU NA AMANI HAIZEKANI KUMUONA MUNGU (EBRANIA 12:14 PART 01:)
PASIPO UTAKATIFU NA AMANI HAIZEKANI KUMUONA MUNGU (EBRANIA 12:14 PART 01:)
От Martin Laizer 2023-10-18 11:55:36 2 8Кб
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-25 05:55:23 0 5Кб
OTHERS
WAKRISTO JIEPUSHENI NA SALAAM MNAYOSALIMIWA NA WAISLAMU
Imekuwa ni desturi kuwasikia, au kumsikia Muislamu, akimsalimia Mkristo, Sam aleykum (سم عليكم)...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:54:09 0 5Кб
NDOA KIBIBLIA
NAJUTA KWA NINI NILIKUBALI KUOLEWA?
Baada ya mwaka mmoja wa ndoa, Merian asema anajuta kwa nini alikubali kuolewa. Merian na Joseph...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:11:44 0 6Кб
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
Biblical Personal Finance: Earning for God's Glory
To paraphrase a question often asked by a popular financial advisor, imagine what the people...
От BIBLICAL FINANCES 2021-12-29 15:33:09 0 8Кб