Ni Sahihi Kumuita Mariamu Mama Wa Mungu?

0
6K

Kwa kuwa Bwana Yesu alipitia katika tumbo la Mariamu je! Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

JIBU: Mariamu alimzaa BWANA kwa namna ya mwili, hivyo wakati Bwana alipokuwa duniani ndio Mariamu alijulikana kama mama wa Yesu, na sio mama wa Mungu. Bwana Yesu alipokuja hapa duniani alikuwa ni Mungu katika mwili lakini hakuja kutafuta kuabudiwa na ndio maana hakuna sehemu yoyote alijiita yeye ni Mungu, zaidi sana alikuwa anawarudisha watu wamuabudu Baba.   Kumbuka Mungu alipouvaa mwili ilimpasa afananishwe na mwanadamu kwa namna zote, azaliwe, ale chakula, asikie maumivu, alie, aone huruma, n.k. kama mwanadamu mwingine yeyote, si ajabu kumuona akiwa na Baba au bibi, au babu au mjomba, lakini haimaanishi kuwa yeye (YESU) yupo chini ya hao wote hapana..

Biblia inatueleza vizuri juu ya jambo hilo tukisoma katika..

Mathayo 22:41 Bwana Yesu alizungumza maneno haya;  

“41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo? 42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi. 43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema, 44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako? 45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe? 46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena”.

Unaona hapo? jibu litakuwa pia hivyo hivyo kwa Mariamu kwamba Yesu atakuwaje mwanawe na wakati bado ni Bwana wake? na yeye ni binti wa Mungu (Kwasababu kama Daudi alikuwa mkubwa kuliko Mariamu aliambiwa hivyo je! si zaidi yeye?).  

Hivyo sisi wote tunaomwamini YESU KRISTO mbele zake ni ndugu na dada, Na yeye akiwa kama Baba yetu. Kwahiyo ni muhimu tujue kutofautisha jinsi Mungu anavyotenda kazi katika ofisi zake tofauti, Mungu anapoonyesha unyenyekevu (kuzaliwa kibinadamu) haimaanishi kuwa mwanadamu yupo juu yake. Hapana anafanya hivyo kutuonyesha sisi njia bora kama watoto wake.  

Ubarikiwe sana.


Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
2 KINGS
Verse by verse explanation of 2 Kings 14
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-03-19 20:30:14 0 5K
NDOA KIBIBLIA
NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE
Mithali 14: 1 ‘Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu...
By GOSPEL PREACHER 2021-12-16 12:09:11 0 8K
Injili Ya Yesu Kristo
MOTO WA KIGENI
Walawi 10:1-2 “Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mtu chetezo chake,...
By GOSPEL PREACHER 2023-06-25 01:00:10 2 8K
OTHERS
MIJADALA YA DINI NI MUHIMU.
Watu wengi katika jamii yetu wanasema kuwa tusiendekeze mijadala ya dini. Wanasema kuwa ni tishio...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:14:33 0 5K
JUDGES
Verse by verse explanation of Judges 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 11:16:35 0 5K