Kwanini Mungu Hakumuua Nyoka, Akamwacha Hawa Ajaribiwe Katika Bustani Ya Edeni?

0
7K

JIBU: Hili ni swali watu wengi wanajiuliza ni Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, badala yake akamwacha Hawa ajaribiwe na yeye?.

Tunapaswa tufahamu wakati mwingine Mungu anaruhusu sisi wanadamu tujaribiwe kwa makusudi maalumu ili tuujue uweza wake na asili yake kwetu sisi na pia tumjue yeye zaidi, kwamfano jaribu kufikiria tungemjuaje kama yeye ni mwokozi kama tusingepotea katika dhambi?, tungejuaje yeye ni mponyaji kama tusingeumwa, tungejuaje yeye ni wa rehema kama tusingeanguka, tungejuaje yeye ni wa neema kama tusingekuwa hatuna haki, tungejuaje yeye ni mwenye msamaha kama tusingekuwa na makosa n.k…

Kumbuka pia sikuzote dhahabu ili ing’ae lazima ipitishwe kwenye moto mkali ijaribiwe na sisi kama watoto wa Mungu ni lazima tujaribiwe na ndio maana Mungu hakumuua shetani. Hata tulipokuwa shuleni, lengo la mwalimu kututungia mitihani migumu sio kutufunya sisi tufeli, hapana bali ni kutuimarisha zaidi ili tuweze kukabiliana na changamoto za mbeleni. Na ndivyo ilivyo kwa Baba yetu wa mbinguni.   Mungu ana makusudi makubwa sana na sisi chini ya jua na ndio maana anatupitisha katika njia hiyo. Tunachopaswa kufahamu ni kuwa siku zote Mungu anatuwazia mawazo yaliyo mema  

Yeremia 29:11 ” Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.”  

Yote haya Mungu kayaruhusu ili kutuwekea msingi mzuri wa maisha yajayo matamu ya umilele yasiyokuwa na mwisho.   Hiyo ndio sababu kwanini Mungu hakumuua nyoka mwanzoni kabisa pale Edeni kabla hajaasi.

Zaburi 103:12 “Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi. 13 Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao. 14 Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi. 15 Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo”.

 

Ubarikiwe sana.


Zoeken
Categorieën
Read More
JOB
Book of Job Explained
Book of Job “Title”: As with other books of the Bible, Job bears the name of the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-02 13:11:05 0 6K
URAFIKI KIBIBLIA
KANUNI 7 ZA KUANZISHA NA KUENDESHA URAFIKI
Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; ….kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 10:47:13 0 6K
NDOA KIBIBLIA
MWANAMUME HAPASWI KUWA MBINAFSI, MCHOYO
Bwana Yesu asifiwe, Amani iwe nawe.Leo napenda tuanze kuangalia mfululizo wa somo hili la,...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 13:35:45 0 5K
Networking
How to grow your marketplace on a budget
Creating a collaborative marketplace is complex. You need suppliers, customers for those...
By Business Academy 2022-09-17 01:57:18 0 5K
JOB
Verse by verse explanation of Job 25
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 13 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:56:56 0 5K