Kwanini Mungu Hakumuua Nyoka, Akamwacha Hawa Ajaribiwe Katika Bustani Ya Edeni?

0
7كيلو بايت

JIBU: Hili ni swali watu wengi wanajiuliza ni Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, badala yake akamwacha Hawa ajaribiwe na yeye?.

Tunapaswa tufahamu wakati mwingine Mungu anaruhusu sisi wanadamu tujaribiwe kwa makusudi maalumu ili tuujue uweza wake na asili yake kwetu sisi na pia tumjue yeye zaidi, kwamfano jaribu kufikiria tungemjuaje kama yeye ni mwokozi kama tusingepotea katika dhambi?, tungejuaje yeye ni mponyaji kama tusingeumwa, tungejuaje yeye ni wa rehema kama tusingeanguka, tungejuaje yeye ni wa neema kama tusingekuwa hatuna haki, tungejuaje yeye ni mwenye msamaha kama tusingekuwa na makosa n.k…

Kumbuka pia sikuzote dhahabu ili ing’ae lazima ipitishwe kwenye moto mkali ijaribiwe na sisi kama watoto wa Mungu ni lazima tujaribiwe na ndio maana Mungu hakumuua shetani. Hata tulipokuwa shuleni, lengo la mwalimu kututungia mitihani migumu sio kutufunya sisi tufeli, hapana bali ni kutuimarisha zaidi ili tuweze kukabiliana na changamoto za mbeleni. Na ndivyo ilivyo kwa Baba yetu wa mbinguni.   Mungu ana makusudi makubwa sana na sisi chini ya jua na ndio maana anatupitisha katika njia hiyo. Tunachopaswa kufahamu ni kuwa siku zote Mungu anatuwazia mawazo yaliyo mema  

Yeremia 29:11 ” Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.”  

Yote haya Mungu kayaruhusu ili kutuwekea msingi mzuri wa maisha yajayo matamu ya umilele yasiyokuwa na mwisho.   Hiyo ndio sababu kwanini Mungu hakumuua nyoka mwanzoni kabisa pale Edeni kabla hajaasi.

Zaburi 103:12 “Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi. 13 Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao. 14 Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi. 15 Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo”.

 

Ubarikiwe sana.


البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
What is a Tithe?
What does the Bible say about tithing Tithing is the practice of setting aside 10% of your...
بواسطة BIBLICAL FINANCES 2021-12-29 14:51:07 0 7كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
KWA NINI WAAMINI WENGI WANATESWA NA VIFUNGO VYA UOVU?
Waamini wengi wana changamoto kuhusu suala zima la uponyaji na kufunguliwa katika vifungo...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:14:48 0 5كيلو بايت
UCHUMBA KIBIBLIA
WACHUMBA 7 WATAKAOSHINDWA
Kutahadharishwa mabaya ni kutayarishwa kwa mazuri“Ni yale mambo...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-06 11:03:29 0 5كيلو بايت
أخرى
Top 2 Types of Voucher in Accounting (With Formats)
  The following points highlight the top two types of voucher in accounting. The types...
بواسطة PROSHABO ACCOUNTING 2022-03-29 20:38:07 0 8كيلو بايت
SPIRITUAL EDUCATION
HAZINA YA MTU
PALIPO NA HAZINA YA MTU NDIPO NA MOYO WAKE UTAKAPOKUWA 
بواسطة Martin Laizer 2023-09-25 06:09:55 0 13كيلو بايت