Kwanini Mungu Hakumuua Nyoka, Akamwacha Hawa Ajaribiwe Katika Bustani Ya Edeni?

0
7K

JIBU: Hili ni swali watu wengi wanajiuliza ni Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, badala yake akamwacha Hawa ajaribiwe na yeye?.

Tunapaswa tufahamu wakati mwingine Mungu anaruhusu sisi wanadamu tujaribiwe kwa makusudi maalumu ili tuujue uweza wake na asili yake kwetu sisi na pia tumjue yeye zaidi, kwamfano jaribu kufikiria tungemjuaje kama yeye ni mwokozi kama tusingepotea katika dhambi?, tungejuaje yeye ni mponyaji kama tusingeumwa, tungejuaje yeye ni wa rehema kama tusingeanguka, tungejuaje yeye ni wa neema kama tusingekuwa hatuna haki, tungejuaje yeye ni mwenye msamaha kama tusingekuwa na makosa n.k…

Kumbuka pia sikuzote dhahabu ili ing’ae lazima ipitishwe kwenye moto mkali ijaribiwe na sisi kama watoto wa Mungu ni lazima tujaribiwe na ndio maana Mungu hakumuua shetani. Hata tulipokuwa shuleni, lengo la mwalimu kututungia mitihani migumu sio kutufunya sisi tufeli, hapana bali ni kutuimarisha zaidi ili tuweze kukabiliana na changamoto za mbeleni. Na ndivyo ilivyo kwa Baba yetu wa mbinguni.   Mungu ana makusudi makubwa sana na sisi chini ya jua na ndio maana anatupitisha katika njia hiyo. Tunachopaswa kufahamu ni kuwa siku zote Mungu anatuwazia mawazo yaliyo mema  

Yeremia 29:11 ” Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.”  

Yote haya Mungu kayaruhusu ili kutuwekea msingi mzuri wa maisha yajayo matamu ya umilele yasiyokuwa na mwisho.   Hiyo ndio sababu kwanini Mungu hakumuua nyoka mwanzoni kabisa pale Edeni kabla hajaasi.

Zaburi 103:12 “Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi. 13 Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao. 14 Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi. 15 Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo”.

 

Ubarikiwe sana.


Search
Categories
Read More
OTHERS
The 20 Versions of the Qur'an today. (7 are recorded in the Hadith.)
The Muslim Claim that the Qur'an is unchanged:No other book in the world can match the...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:43:46 0 5K
DANIEL
DANELI 7
Jina la BWANA wetu YESU KRISTO lihimidiwe.   Katika sura zilizotangulia (yaani...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-05 23:55:37 0 12K
Injili Ya Yesu Kristo
Ushuhuda wa Victoria Juu ya Kuzimu
Huu ni ufupisho wa ushuhuda wa Victoria Nehale Nilizaliwa na kuishi Namibia maisha yangu yote;...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:40:22 0 5K
OTHERS
How an Atheist Found God
A personal account from an atheist who was convinced no god exists, and what facts led to God....
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:43:58 0 6K
MAHUSIANO KIBIBLIA
SEHEMU YA 1: MISINGI YA KIIMANI KATIKA MAHUSIANO YA UCHUMBA HADI NDOA
Bwana asifiwe!! Unaweza kusoma SEHEMU YA 2, SEHEMU YA 3, SEHEMU YA 4 au SEHEMU YA 5 ya somo...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 11:37:57 0 5K