Kwanini Mungu Hakumuua Nyoka, Akamwacha Hawa Ajaribiwe Katika Bustani Ya Edeni?

0
6K

JIBU: Hili ni swali watu wengi wanajiuliza ni Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, badala yake akamwacha Hawa ajaribiwe na yeye?.

Tunapaswa tufahamu wakati mwingine Mungu anaruhusu sisi wanadamu tujaribiwe kwa makusudi maalumu ili tuujue uweza wake na asili yake kwetu sisi na pia tumjue yeye zaidi, kwamfano jaribu kufikiria tungemjuaje kama yeye ni mwokozi kama tusingepotea katika dhambi?, tungejuaje yeye ni mponyaji kama tusingeumwa, tungejuaje yeye ni wa rehema kama tusingeanguka, tungejuaje yeye ni wa neema kama tusingekuwa hatuna haki, tungejuaje yeye ni mwenye msamaha kama tusingekuwa na makosa n.k…

Kumbuka pia sikuzote dhahabu ili ing’ae lazima ipitishwe kwenye moto mkali ijaribiwe na sisi kama watoto wa Mungu ni lazima tujaribiwe na ndio maana Mungu hakumuua shetani. Hata tulipokuwa shuleni, lengo la mwalimu kututungia mitihani migumu sio kutufunya sisi tufeli, hapana bali ni kutuimarisha zaidi ili tuweze kukabiliana na changamoto za mbeleni. Na ndivyo ilivyo kwa Baba yetu wa mbinguni.   Mungu ana makusudi makubwa sana na sisi chini ya jua na ndio maana anatupitisha katika njia hiyo. Tunachopaswa kufahamu ni kuwa siku zote Mungu anatuwazia mawazo yaliyo mema  

Yeremia 29:11 ” Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.”  

Yote haya Mungu kayaruhusu ili kutuwekea msingi mzuri wa maisha yajayo matamu ya umilele yasiyokuwa na mwisho.   Hiyo ndio sababu kwanini Mungu hakumuua nyoka mwanzoni kabisa pale Edeni kabla hajaasi.

Zaburi 103:12 “Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi. 13 Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao. 14 Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi. 15 Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo”.

 

Ubarikiwe sana.


Tafuta
Vitengo
Soma Zaidi
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 32
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 62 questions at the...
Kwa THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:05:04 0 5K
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 24
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
Kwa THE HOLY BIBLE 2022-04-02 02:01:48 0 5K
STANDARD 7
STANDARD 7
List of all subjects for the standard 7 class
Kwa PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:22:31 0 5K
OTHERS
Back to Basics: Dealing with demonic dreams
Ugh. While I totally understand the despair, I would like to offer an alternative response:...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 11:01:41 0 5K
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 54 questions at the...
Kwa THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:26:28 0 5K