Je! Kiongozi Wa Dini Anao uwezo Wa Kusamehe Dhambi?

0
6K

SWALI: Je! Ni sahihi kwenda kumfuata kiongozi wa dini kwa mfano Padre na kumpigia magoti kumweleza dhambi zako?.kwasababu imeandikwa “Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; (Yohana 20:23)”

JIBU: Kwa kuongezea hapo Bwana Yesu pia alisema..

Mathayo 16:15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? 16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. 17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni. 18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. 19 NAMI NITAKUPA WEWE FUNGUO ZA UFALME WA MBINGUNI; NA LOLOTE UTAKALOLIFUNGA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGWA MBINGUNI, NA LOLOTE UTAKALOLIFUNGUA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGULIWA MBINGUNI.”

Hapo tunaona Petro alipewa funguo za ufalme wa mbinguni za kufunga na kufungua,(ambazo ni sawasawa tu na kumwondolea na kumfungia mtu dhambi) na vivyo hivyo na mitume wengine wote waliosalia walipewa funguo hizo hizo, lakini haikuwa na maana kuwa “wanao uwezo wa kumwondolea mtu dhambi kwa kumtamkia tu basi” hapana! bali walipewa “FUNGUO” za kumfanya mtu kuondolewa dhambi zake(UELEWA),, na ndio maana Petro na mitume wengine walipowahubiria watu na kuamini moja kwa moja waliwaambia WATUBU na WAKABATIZWE KILA MMOJA WAO KWA JINA LA YESU KRISTO ili dhambi zao ziondolewe (Matendo 2:38) lakini hawakuwaambia..”Njooni sisi tumepewa uwezo wa kuwaondolea dhambi zenu hivyo pokeeni msamaha”….

Unaona hapo huo ufunguo ni UFUNUO/UELEWA wa jinsi ya kufanya dhambi za mtu ziondolewe, Na ndio huo wa kumuhubiria mtu atubu, kisha akishatubu akabatizwe, hapo ndipo dhambi zake zitakuwa zimeondolewa.

Lakini Papa na Mapadre, na baadhi ya viongozi wengine wa kidini hawafanyi kama mitume walivyofanya bali wao wanawatamkia tu watu kwamba wamesamehewa dhambi zao basi, bila kufuata mwongozo sahihi kwa kisingizio cha hayo maandiko ya kwamba wao wamepewa hayo mamlaka….(kutokana na kukosa UFUNUO wa Roho Mtakatifu ndani yao wanayatafsiri maandiko kwa akili zao ili kutimiza matakwa yao wenyewe.) Mungu atusaidie. Kwahiyo kiongozi yeyote wa kidini akikwambia umesamehewa dhambi zako, pasipo toba binafsi na ubatizo sahihi matamshi yake ni batili yakatae.

Ubarikiwe sana.

Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
OTHERS
NANI ALIYE TOLEWA KAFARA, ISHMAEL AU ISAKA?
Kwenye Mwanzo 22:1-18, je inawezekana kuwa mvulana ambaye Abraham alikaribia kumtoa kafara awe ni...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:41:15 0 5K
Religion
HATUA ZA KUINUKA BAADA YA KUANGUKA
Bwana Yesu asifiwe! Huna sababu ya kubakia hapo chini baada ya kuanguka majaribuni. Kwa...
By GOSPEL PREACHER 2021-09-04 07:33:04 1 6K
HOLY BIBLE
FAHAMU UWEZO WA DAMU YA YESU KRISTO
Ukweli ni kwamba katika damu ya Yesu Kristo kunapatikana zaidi ya mambo manne...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:24:49 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
Msikilizeni Israel, Baba yenu!
Mstari wa Msingi:- Mwanzo 49:1-2 “Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili...
By GOSPEL PREACHER 2022-04-01 08:36:48 0 7K
UCHUMBA KIBIBLIA
UCHUMBA NI NINI? NA NDOA NI NINI?
Shalom, wapendwa,Katika somo letu leo nataka tuangalie vitu hivi viwili, mahusiano ya uchumba na...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 13:06:36 0 7K