Je! Kiongozi Wa Dini Anao uwezo Wa Kusamehe Dhambi?

0
6كيلو بايت

SWALI: Je! Ni sahihi kwenda kumfuata kiongozi wa dini kwa mfano Padre na kumpigia magoti kumweleza dhambi zako?.kwasababu imeandikwa “Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; (Yohana 20:23)”

JIBU: Kwa kuongezea hapo Bwana Yesu pia alisema..

Mathayo 16:15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? 16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. 17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni. 18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. 19 NAMI NITAKUPA WEWE FUNGUO ZA UFALME WA MBINGUNI; NA LOLOTE UTAKALOLIFUNGA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGWA MBINGUNI, NA LOLOTE UTAKALOLIFUNGUA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGULIWA MBINGUNI.”

Hapo tunaona Petro alipewa funguo za ufalme wa mbinguni za kufunga na kufungua,(ambazo ni sawasawa tu na kumwondolea na kumfungia mtu dhambi) na vivyo hivyo na mitume wengine wote waliosalia walipewa funguo hizo hizo, lakini haikuwa na maana kuwa “wanao uwezo wa kumwondolea mtu dhambi kwa kumtamkia tu basi” hapana! bali walipewa “FUNGUO” za kumfanya mtu kuondolewa dhambi zake(UELEWA),, na ndio maana Petro na mitume wengine walipowahubiria watu na kuamini moja kwa moja waliwaambia WATUBU na WAKABATIZWE KILA MMOJA WAO KWA JINA LA YESU KRISTO ili dhambi zao ziondolewe (Matendo 2:38) lakini hawakuwaambia..”Njooni sisi tumepewa uwezo wa kuwaondolea dhambi zenu hivyo pokeeni msamaha”….

Unaona hapo huo ufunguo ni UFUNUO/UELEWA wa jinsi ya kufanya dhambi za mtu ziondolewe, Na ndio huo wa kumuhubiria mtu atubu, kisha akishatubu akabatizwe, hapo ndipo dhambi zake zitakuwa zimeondolewa.

Lakini Papa na Mapadre, na baadhi ya viongozi wengine wa kidini hawafanyi kama mitume walivyofanya bali wao wanawatamkia tu watu kwamba wamesamehewa dhambi zao basi, bila kufuata mwongozo sahihi kwa kisingizio cha hayo maandiko ya kwamba wao wamepewa hayo mamlaka….(kutokana na kukosa UFUNUO wa Roho Mtakatifu ndani yao wanayatafsiri maandiko kwa akili zao ili kutimiza matakwa yao wenyewe.) Mungu atusaidie. Kwahiyo kiongozi yeyote wa kidini akikwambia umesamehewa dhambi zako, pasipo toba binafsi na ubatizo sahihi matamshi yake ni batili yakatae.

Ubarikiwe sana.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
Injili Ya Yesu Kristo
DALILI ZA KUMJUA MTUMISHI/NABII WA UONGO.
Ndugu msomaji na mwanadamu uliyeumbwa kwa mfano wa sura ya MUNGU na siyo ya shetani, MUNGU huyu...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:52:58 0 6كيلو بايت
HOLY BIBLE
Will more people go to heaven or to hell?
The question of whether there are more people in heaven or hell is answered by Jesus Himself in...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:21:07 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
NAMNA SHETANI ANAVYOTUMIA ROHO YA USAHULIFU KUHARIBU MAISHA YA WAAMINI
  Shalom, katika waraka huu wa Desemba 2016 nimeona ni vema kukumbusha juu ya jambo hili...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:31:32 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:33:21 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
MATOKEO YA DHAMBI YA UZINZI/UASHERATI KWA MTU ALIYEOKOKA.
Nakusalimu katika jina la Bwana mwezi huu wa tisa. Katika mwezi huu nimesukumwa ndani yangu...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:49:03 0 5كيلو بايت