Je! ni sahihi kuning’iniza picha nyumbani mwako kama ya Yesu?

0
6كيلو بايت

Swali linaendelea…maana imeandikwa kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. “

Sasa naomba kufahamu kufanya hivyo ni makosa?


JIBU: kwa kulijibu hili swali tumalizie kusoma mstari huo..

Kutoka 20:4-5″ Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”…

Sasa tunaona katika huo mstari wa tano msisitizo umewekwa pale katika neno “USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA”, lakini sio kwamba ukiweka picha yoyote kama ya Yesu nyumbani mwako ni vibaya hapana! unaweza kuweka picha yoyote upendayo ilimradi iwe ni njema,

Maana tukisema tusiweke picha yoyote basi hata tunaponing’iniza picha zetu wenyewe ukutani majumbani mwetu tunafanya vibaya kwasababu maandiko yanasema usijifanyie mfano wa kitu chochote sio tu kilicho juu mbinguni bali hata kilichopo chini duniani.

Unaona hapo msisitizo ni kwamba unapoweka picha yoyote au sanamu yoyote hupaswi kuiabudu wala kuisujudia kwa kufanya hivyo ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Lakini leo hii kuna baadhi ya watu,na dini na madhehebu yanaabudu sanamu za Yesu na bikira Mariamu au watakatifu waliokufa zamani za kale hao ni dhahiri kuwa wanamwabudu shetani aidha kwa kujua au kwa kutokujua.

Ikiwa wewe ni mkatoliki na unayo sanamu ya Yesu au sanamu ya bikira Maria nyumbani mwako, nashauri iondoe haraka sana, kwasababu dini hiyo inaahusisha ibada zao na sanamu, vinginevyo utamtia Mungu wivu na kujikuta umeenda Jehanamu.

Lakini kama picha ipo kwa ajili ya urembo au kwa ajili ya kufikisha tu ujumbe fulani katika mazingira yanayokuzunguka au nyumbani kwako, wala husujudii wala kuabudu basi hakuna shida yoyote. Zingatia tu hilo neno ”USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA’ kwasababu yeye ni Mungu mwenye wivu.

Biblia inasema;

1 Wakorintho 10:14

[14]Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.
[15]Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo.

Ubarikiwe sana.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 11
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 51 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-02-05 13:10:21 0 6كيلو بايت
2 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 32 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-02-05 16:04:51 0 5كيلو بايت
OTHERS
Je, Muhammad Ametabiriwa Kwenye Biblia?
SEHEMU YA KWANZA Waislamu wanashikilia kwamba Muhammad alitabiriwa kwenye Biblia. Andiko lao kuu...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:29:25 0 6كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
WHY MASTURBATION IS A SIN…..Please read this!
To start with, masturbation is self service by which one derives pleasure; it’s a sexual...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:30:57 0 5كيلو بايت
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 33
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-23 05:34:22 0 7كيلو بايت