Je! ni sahihi kuning’iniza picha nyumbani mwako kama ya Yesu?

0
6كيلو بايت

Swali linaendelea…maana imeandikwa kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. “

Sasa naomba kufahamu kufanya hivyo ni makosa?


JIBU: kwa kulijibu hili swali tumalizie kusoma mstari huo..

Kutoka 20:4-5″ Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”…

Sasa tunaona katika huo mstari wa tano msisitizo umewekwa pale katika neno “USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA”, lakini sio kwamba ukiweka picha yoyote kama ya Yesu nyumbani mwako ni vibaya hapana! unaweza kuweka picha yoyote upendayo ilimradi iwe ni njema,

Maana tukisema tusiweke picha yoyote basi hata tunaponing’iniza picha zetu wenyewe ukutani majumbani mwetu tunafanya vibaya kwasababu maandiko yanasema usijifanyie mfano wa kitu chochote sio tu kilicho juu mbinguni bali hata kilichopo chini duniani.

Unaona hapo msisitizo ni kwamba unapoweka picha yoyote au sanamu yoyote hupaswi kuiabudu wala kuisujudia kwa kufanya hivyo ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Lakini leo hii kuna baadhi ya watu,na dini na madhehebu yanaabudu sanamu za Yesu na bikira Mariamu au watakatifu waliokufa zamani za kale hao ni dhahiri kuwa wanamwabudu shetani aidha kwa kujua au kwa kutokujua.

Ikiwa wewe ni mkatoliki na unayo sanamu ya Yesu au sanamu ya bikira Maria nyumbani mwako, nashauri iondoe haraka sana, kwasababu dini hiyo inaahusisha ibada zao na sanamu, vinginevyo utamtia Mungu wivu na kujikuta umeenda Jehanamu.

Lakini kama picha ipo kwa ajili ya urembo au kwa ajili ya kufikisha tu ujumbe fulani katika mazingira yanayokuzunguka au nyumbani kwako, wala husujudii wala kuabudu basi hakuna shida yoyote. Zingatia tu hilo neno ”USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA’ kwasababu yeye ni Mungu mwenye wivu.

Biblia inasema;

1 Wakorintho 10:14

[14]Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.
[15]Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo.

Ubarikiwe sana.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
OTHERS
JE, MUHAMMAD ALIROGWA?
Leo napenda Kumnukuu Mwalimu wangu Daniel Mwankemwa katika majawapo ya Makala ambayo anaelezea...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:53:13 0 5كيلو بايت
Religion
Sadaka inayomgusa Mungu
Nianze kwa kuwashukuru na kuwapongeza wasomaji wa makala hii, najua kuna faida nyingi za kiroho,...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-08-25 09:39:38 0 9كيلو بايت
MASWALI & MAJIBU
Je! kuna dhambi kubwa na ndogo?
SWALI: Naomba kufahamu Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-06-13 00:12:35 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
HAKUNA PETE YA NDOA KIBIBLIA
Ni muhimu kufahamu kuwa neno pete limetajwa katika Biblia. Sasa kama neno hili limetajwa katika...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:40:17 0 6كيلو بايت
OTHERS
UTATA: NUHU WA QURAN NI TOFAUTI NA NUHU WA BIBLIA
Ndugu Msomaji: Siku zote Waislam huwa mnatutambia kuwa, Quran ni kitabu kilichoeleza kila...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:30:49 0 5كيلو بايت