Je! ni sahihi kuning’iniza picha nyumbani mwako kama ya Yesu?

0
6K

Swali linaendelea…maana imeandikwa kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. “

Sasa naomba kufahamu kufanya hivyo ni makosa?


JIBU: kwa kulijibu hili swali tumalizie kusoma mstari huo..

Kutoka 20:4-5″ Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”…

Sasa tunaona katika huo mstari wa tano msisitizo umewekwa pale katika neno “USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA”, lakini sio kwamba ukiweka picha yoyote kama ya Yesu nyumbani mwako ni vibaya hapana! unaweza kuweka picha yoyote upendayo ilimradi iwe ni njema,

Maana tukisema tusiweke picha yoyote basi hata tunaponing’iniza picha zetu wenyewe ukutani majumbani mwetu tunafanya vibaya kwasababu maandiko yanasema usijifanyie mfano wa kitu chochote sio tu kilicho juu mbinguni bali hata kilichopo chini duniani.

Unaona hapo msisitizo ni kwamba unapoweka picha yoyote au sanamu yoyote hupaswi kuiabudu wala kuisujudia kwa kufanya hivyo ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Lakini leo hii kuna baadhi ya watu,na dini na madhehebu yanaabudu sanamu za Yesu na bikira Mariamu au watakatifu waliokufa zamani za kale hao ni dhahiri kuwa wanamwabudu shetani aidha kwa kujua au kwa kutokujua.

Ikiwa wewe ni mkatoliki na unayo sanamu ya Yesu au sanamu ya bikira Maria nyumbani mwako, nashauri iondoe haraka sana, kwasababu dini hiyo inaahusisha ibada zao na sanamu, vinginevyo utamtia Mungu wivu na kujikuta umeenda Jehanamu.

Lakini kama picha ipo kwa ajili ya urembo au kwa ajili ya kufikisha tu ujumbe fulani katika mazingira yanayokuzunguka au nyumbani kwako, wala husujudii wala kuabudu basi hakuna shida yoyote. Zingatia tu hilo neno ”USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA’ kwasababu yeye ni Mungu mwenye wivu.

Biblia inasema;

1 Wakorintho 10:14

[14]Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.
[15]Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo.

Ubarikiwe sana.

Tafuta
Vitengo
Soma Zaidi
OTHERS
SHETANI NA MAJINI MACHAFU YASILIMU NA KUWA WAISLAM
1. Mtume Muhammad akutana na Majini usiku na kuyafundisha Quran.2. Shetani na yeye aingia...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:58:59 0 5K
HOLY BIBLE
Do you have to be baptized to be filled with the Holy Spirit?
No, you do not have to be baptized to be filled with the Holy Spirit. To prove this all we have...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:39:59 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
KWARESMA IPO KIBIBLIA
KWARESMA IPO KIMAANDIKO?       Kwaresma ni nini?..Je! Kwaresma ipo katika...
Kwa Martin Laizer 2025-03-11 02:12:09 2 2K
SPIRITUAL EDUCATION
NI NINI KITAKACHOTUTENGA NA UPENDO YESU KRISTO?
NI NINI KITAKACHOTUTENGA NA UPENDO YESU KRISTO?WARUMI 8:35-39
Kwa Martin Laizer 2023-09-30 15:42:48 1 16K
SPIRITUAL EDUCATION
INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA* .
INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA* .
Kwa Martin Laizer 2023-10-17 20:10:29 7 7K